Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 11 2023-08-29

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NORAH W. MZERU sliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo la uhaba wa Hosteli kwa wanafunzi wa Elimu ya Juu wanaosoma katika Vyuo vya Mkoa wa Morogoro?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA, Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Norah Waziri Mzeru Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inafanya juhudi mbalimbali katika kutatua tatizo la uhaba wa hosteli kwa wanafunzi wanaosoma katika vyuo vikuu hapa nchini vikiwemo Vyuo vya Mkoa wa Morogoro. Kwa sasa hosteli zilizopo katika vyuo vikuu vya Mzumbe na Sokoine zina uwezo wa kulaza jumla ya wanafunzi 7571. Ikiwa Mzumbe ni wanafunzi 3742 na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo ni wanafunzi 3829.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo wanafunzi ambao hawapati nafasi za malazi katika hosteli za vyuo wamekuwa wakipata malazi katika hosteli zinazomilikiwa na watu binafsi katika maeneo yaliyokaribu na vyuo.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua ongezeko la uhitaji wa malazi kwa wanafunzi katika vyuo vikuu vya serikali vikiwemo vyuo vya Mkoa wa Morogoro, Serikali imekamilisha ujenzi wa hosteli 4 zenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 1024 katika Chuo Kikuu cha Mzumbe na zimeanza kutumika kuanzia mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, aidha kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali kupitia Mradi wa Higher Education for Economic Transformation yaani HEET imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Hosteli moja yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 600 katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo Kampasi ya Mazimbu Morogoro. Nashukuru.