Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Aliuliza: - Je, kwa nini kumekuwa na ugumu wa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi wanapojiunga na elimu ya juu?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Shule binafsi ni wadau wakubwa sana wa elimu katika Taifa hili la Tanzania lakini imekuwa mara nyingi vijana hawa wakifika elimu ya juu wanakosa mikopo au kupata chini ya 40% hatuoni kwamba tunawaonea, watoto wengine wamesomeshwa kwa msaada wakiwemo yatima, kuwazuia kuendelea na elimu ya juu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Serikali haioni sasa kuna umuhimu watoto wa nchi hii wote wapate mikopo flatrate yani mikopo ya aina moja bila kugawa kwa asilimia ili watoto wote wapate usawa katika Taifa hili? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge Mwakagenda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha eleza kwenye majibu ya swali la msingi kwamba utoaji wa mikopo yetu hauzingatii mwanafunzi amesoma katika shule gani, iwe shule ya umma au shule ya Serikali ilimradi wamekidhi vile vigezo wanafunzi hao wanawajibika kupata hiyo mikopo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli anachozungumza Mheshimiwa Mbunge kwamba kumekuwa na changamoto wakati mwingine wakupata asilimia chache sana ya mikopo hii. Tunafahamu kuwa juhudi za Serikali zakuongeza wigo wa kupata mikopo hii kwa kuzingatia bajeti yetu ya Serika bado zinaendelea.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako tukufu Serikali imeendelea kuongeza fedha za mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kutoka shilingi bilioni 464 mwaka 2021/2022 mpaka shilingi bilioni 738 mwaka 2023/2024. Ni matumaini yetu kuwa ongezeko hili la bajeti litahakikisha kwamba wanafunzi wengi wanapata mikopo na kwa kiasi kikubwa cha mikopo.

Mheshimiwa Spika, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, vilevile Serikali imeendelea kufanya juhudi ya kutafuta wadau mbalimbali wa kuweza kuongeza nguvu. Mpaka sasa tunavyozungumza taasisi yetu ya Benki ya NMB katika mwaka wa fedha uliopita iliweza kutenga shilingi bilioni 200 kwa ajili ya mikopo hii. Na katika mwaka huu vilevile itatenga fedha hizo.

Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali ikiwa ni kuhakikisha kwamba kila mwanafunzi wa elimu ya juu anapata mkopo na anapata mkopo katika kile kiasi ambacho kinahitajika. Nashukuru sana.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Aliuliza: - Je, kwa nini kumekuwa na ugumu wa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi wanapojiunga na elimu ya juu?

Supplementary Question 2

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya kati ambao wanapata diploma na vyeti hapa nchini kwetu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Saputu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti yetu ya 2023/2024 jambo hili lilizungumzwa bayana katika Bajeti Kuu ya Serikali. Serikali imetenga fedha kwa ajili ya utoaji mikopo kwa vyuo hivi vya kati na programme hii itaanza mwaka huu wa fedha.

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Aliuliza: - Je, kwa nini kumekuwa na ugumu wa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi wanapojiunga na elimu ya juu?

Supplementary Question 3

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mheshimiwa Waziri huoni umuhimu sasa wa Serikali kufanya mapitio ya sheria ya hii Bodi ya Mikopo ili kuweza kutatua changamoto nyingi ambazo watoto wa Kitanzania wanazipata kupata mikopo ya elimu ya juu? Nashukuru. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Tweve kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mradi wetu wa Higher Education for Economic Transformation tumetenga fedha kwa ajili ya kufanya mapitio. Tunafahamu sheria hii ya Bodi ya Mikopo imeanza toka 2004 ni miaka 19 sasa toka sheria hii ianze. Kwa hiyo, hivi sasa tunafanya mapitio ili kuangalia vigezo namna gani ya kuweza ku-update information zetu lakini vilevile namna ya utoaji wa mikopo hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimuondoe wasi wasi Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako tukufu mpaka kufika mwisho wa mwaka huu wa fedha shughuli hii itakuwa imekamilika na bodi yetu sasa itakuwa na sheria pamoja na miongozo ambayo itaendana sawa na kasi ya sasa.

Name

Dr. Paulina Daniel Nahato

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Aliuliza: - Je, kwa nini kumekuwa na ugumu wa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi wanapojiunga na elimu ya juu?

Supplementary Question 4

MHE. PAULINA D. NAHATO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuwapatia mikopo wanafunzi wote wenye ulemavu wa aina yoyote katika vyuo vyetu vikuu kwa 100%?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Nahato kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hivi sasa kigezo kimoja wapo cha wanafunzi kupata mikopo ni wale wenye ulemavu naomba nimuondoe wasi wasi Mheshimiwa Mbunge watoto wetu vijana wetu wenye ulemavu wanapata mikopo kwa 100% na huo ndiyo mpango wa Serikali.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Aliuliza: - Je, kwa nini kumekuwa na ugumu wa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi wanapojiunga na elimu ya juu?

Supplementary Question 5

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini sasa Serikali itaanzisha revolving fund ikiwa na maana kwamba zile fedha zinazokusanywa ziwekwe kwenye mfuko ambao ni fedha lindwa? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Wambura amezungumzia swala la revolving fund kama nilivyoeleza kwenye swali la nyongeza la Mheshimiwa Tweve nadhani kwamba hivi sasa tunafanya mapitio ya sheria ile. Katika mapitio yale tutakwenda kuangalia hayo mambo yote pamoja na kuangalia kama mfuko unaweza kujiendesha lakini vilevile katika kujiendesha katika taratibu za kibenki ikiwemo na hii revolving fund. Kwa hiyo, nimuondoe wasi wasi jambo hili linafanyiwa kazi.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Aliuliza: - Je, kwa nini kumekuwa na ugumu wa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi wanapojiunga na elimu ya juu?

Supplementary Question 6

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, NMB kama mdau wa elimu ameandaa shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kutoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu lakini mikopo hii itatolewa kwa wale wanafunzi ambao wazazi wao ni wafanyakazi. Je, kuna mkakati gani wa kuhakikisha wale wanafunzi wanaohitaji mikopo ambao wazazi wao siyo watumishi wanapata mikopo kwa asilimia zote?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Migilla kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli wenzetu wa NMB walitenga fedha shilingi bilioni 200 katika mwaka wa fedha uliopita na mwaka huu watatenga tena kwa ajili ya kuendelea na zoezi hili. Nimuondoe wasi wasi Mheshimiwa Mbunge pamoja na kigezo kile cha mzazi awe ni mtumishi lakini vilevile tumeweka kigezo cha mzazi kuwa mkulima. Ilimradi amejiunga au yupo ndani ya chama cha ushirika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo wazazi wote ambao ni wafanyakazi lakini wazazi wote ambao ni wakulima au wale ambao wako katika vyama mbalimbali wanahusika na mikopo hii na tutakwenda kufanya review kwa kadiri mahitaji yatakavyohitajika, nashukuru.