Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 10 2023-08-29

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Aliuliza: -

Je, kwa nini kumekuwa na ugumu wa upatikanaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi wanapojiunga na elimu ya juu?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda kama ifuatavyo: -

Mheshimwa Spika, mikopo inayotolewa na Serikali kupitia Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inawalenga vijana wenye sifa za kitaaluma za kujiunga na taasisi za elimu ya juu lakini hawana uwezo wa kumudu gharama za elimu.

Mheshimwa Spika, aidha, upangaji na utoaji mikopo unaongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo Sura 178 kwa kuzingatia sifa za msingi ambazo ni: awe Mtanzania; awe amepata udahili wa masomo ya shahada au stashahada katika taasisi inayotambuliwa na Serikali; asiwe na vyanzo vingine vinavyogharamia masomo yake; na kwa wanaoendelea na masomo ya mwaka wa pili, watatu na kuendelea, wawe wamefaulu kuendelea na masomo yao katika mwaka unaofuata.

Mheshimwa Spika, Kila mwaka bodi huandaa mwongozo unaopaswa kuzingatiwa na waombaji na kuweka masharti ya utoaji mikopo kwa mwaka husika. Pamoja na vigezo vilivyotajwa, mwongozo hueleza taratibu za kufuata wakati wa kuomba mkopo pasipo kuangalia mwanafunzi kasoma shule ya binafsi au ya umma.

Mheshimiwa Spika, iwapo muomboji atafuata maelezo yote kama yalivyo katika mwongozo wa mwaka husika na akawa ana vigezo vyote, hatutegemei pawepo na ugumu wowote katika kupata mkopo hata kama alisoma shule binafsi. Nashukuru.