Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Ofisi ya Wilaya ya TANESCO – Kibiti?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Pamoja na maelezo mazuri ya Serikali nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kweli anasema kuna mitandao ambayo inatumika kuhudumiwa na TANESCO lakini Kibiti ni moja ya mkoa ambao uko Kusini mwa Mkoa wa Pwani ambapo kuna mikoa minne; Mkuranga, Mafia pamoja na Rufiji. Sasa hatuoni umuhimu wa kujenga kituo kikubwa sana kwa sababu hapo ni centre ya mikoa ya Kusini ya Mkoa wa Pwani, kituo kikubwa ambacho wananchi wataweza kufika sababu sio vijiji vyote ambavyo wanaweza kufikiwa na mambo ya mtandao? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nashukuru, kama nilivyoeleza kwenye jibu la msingi, tunaendelea kufanya tathmini kwenye paragraph ya kwanza. Nimesema kwa umahususi wa Kibiti kwa ajili ya kuona namna ambavyo tutafanya ili kujenga ofisi hii ili iweze kuhudumia maeneo ya Kibiti lakini na maeneo mengine ya Jirani.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Ofisi ya Wilaya ya TANESCO – Kibiti?

Supplementary Question 2

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante, Miji wa Iringa ni kivutio cha utalii Kusini na katikati ya mji tumeboresha sana majengo yetu. Kuna jengo la TANESCO la Ofisi ya Mkoa ambalo limetelekezwa muda mrefu, ni lini mtalimalizia ili liendelee nalo kuchangia uvutiaji wa Kusini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Katika maeneo yote ambayo majengo hayajakamilika ni swala la kibajeti na tunaendelea kujikusanya kwenye fedha na kutanguliza vipaumbele lakini nimhakikishie Mheshimiwa Jesca kwamba jengo hilo pia litakamilishwa ili liweze kuwahudumia wananchi lakini kama ulivyosema liwe kivutio cha utalii Iringa.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Ofisi ya Wilaya ya TANESCO – Kibiti?

Supplementary Question 3

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wilaya ya Kahama ina Halmashauri tatu na hivyo kusababisha changamoto ya kupata huduma kwa wakati. Lini sasa Serikali inampango wa kuanzisha Mkoa wa ki-TANESCO katika wilaya ya Kahama ili isaidie kutoa huduma kwenye maeneo yale? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kweli Wilaya ya Kahama inazo Halmashauri tatu na sisi tunayo Ofisi ya Kiwilaya ya TANESCO kama zilivyokuwa ofisi nyingine za Serikali na tunachokifanya ni kuendelea kupeleka huduma kwa wananchi kwa kufungua ofisi ndogo au viunga kwenye maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, jambo la kufungua Ofisi ya Kimkoa ya Ki-TANESCO tunaendelea kulitizama kwa sababu zinazo viwango na grade mbalimbali na zitakapokuwa zimekamilika tutakamilisha jambo hilo kwa ajili ya huduma kwa wananchi.