Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 8 2023-08-29

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Ofisi ya Wilaya ya TANESCO – Kibiti?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa umahususi na umuhimu wa Wilaya ya TANESCO Kibiti, TANESCO inafanya tathmini ya gharama kuangalia namna ya kujenga jengo lake la ofisi ili kuepuka kuendelea na ofisi iliyopo sasa ambayo ni ya kupanga.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kutokana na maendeleo makubwa ya teknolojia, kwa sasa huduma nyingi zinatolewa kwa njia ya mtandao. Aidha, programu kama vile NIKONEKT, NIHUDUMIE, kununua umeme (LUKU) na nyinginezo zimeanzishwa ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wateja bila kulazimika kwenda ofisi za TANESCO. Aidha, pamoja na faida nyingine programu hizi zimesaidia kuondoa vishoka waliokuwa wanawalaghai wateja katika ofisi za TANESCO.

Mheshimiwa Spika, shirika limeelekeza fedha nyingi katika kuanzisha na kuboresha huduma zinazotolewa kwa njia ya mtandao. Sambamba na hili, shirika linaendelea kuanzisha viunga/ofisi ndogo zitakazokuwa karibu zaidi na wananchi ili kuwahudumia kwa haraka kwa huduma chache ambazo hazipatikani kwa mtandao kwa sasa. Katika Wilaya ya Kibiti, TANESCO imeanzisha viunga viwili katika maeneo ya Hanga na Bungu ili kusogeza huduma kwa wateja. Ahsante.