Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. lakini barabara inayofanana na Gairo kwenda Nongwe ni barabara ambayo inaanzia Ruaha Mbuyuni – Malolo – Mlunga – Reli Ng’ombe mpaka Kibakwe – Mpwapwa. Barabara hii imeshapitishwa na RCC kwa miaka miwili sasa; Je, nini kauli ya Serikali?

Mheshimiwa Spika, kutokupitisha barabara hii kwa kadiri ya maombi ya RCC mkoa wa Morogoro; Je, Serikali haioni kwamba inawapotezea haki wananchi hawa ambao wanasafiri mwendo zaidi ya kilomita 400 kufika Mpwapwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kwa pamoja ya Mheshimiwa Londo Mbunge wa Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii inaunganisha mikoa ya Morogoro, Iringa na Dodoma na Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba kwa sasa barabara hii inahudumiwa na wenzetu wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini, na atakuwa pia anaelewa kwamba baada ya kupokea maombi kuipandisha barabara hii ili ihudumiwe na TANROADS, wataalamu wameshaitembelea ili kufanyia tathmini na kuona kama inakidhi vigezo vya kuhamishiwa TANROADS. Kwa hiyo tayari maombi yameshafika Wizarani kwa ajili ya kufanyiwa tathmini na maamuzi, na baada ya hapo tutawajulisha kama imekidhi vigezo ili iweze kupanda hadhi, ahsante. (Makofi)

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Barabara ya kwenda Ruaha

kutoka Iringa Mjini iliahidiwa kwamba tutatangaza mwezi wa sita, mpaka sasa haijatangazwa; je, tutatangaza lini? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kulikuwa na taratibu zilikuwa bado hazijakamilika lakini zinakamilika, na baada ya hapo hiyo barabara itatangazwa ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, tarehe 5, mwezi wa Nane Wizara ilisaini barabara ya kutoka Ifakara kwenda Mbingu na baadaye Mlimba. Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara hiyo itaanza kujengwa mara tu tutakapokuwa tumekamilisha taratibu zote ikiwa ni pamoja na mkandarasi kuanza kufanya mobilization, yaani kuandaa vifaa kwa ajili ya kuanza kuijenga hiyo barabara. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika; je, Serikali imefikia hatua gani katika maandalizi ya kuijenga Barabara ya Hydom – Mogitu kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara hiyo ilishafanyiwa usanifu na Serikali inatafuta fedha kuijenga hiyo Barabara ya Hydom Mogitu kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Spika, Barabara ya Msongola – Mbande kilometa 4.95, ujenzi wa kilometa 1.5 una suasua. Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha ujenzi huo pamoja na kilometa 3.45 za kumalizia kwa lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba tu nichukue nafasi hii kumuelekeza Meneja wa TANROADS wa Mkoa wa Dar es Salaam kumsisitiza mkandarasi kwa sababu yuko site ili barabara hiyo iweze kukamilika ili tuondokane na hiyo vumbi ambayo ina kilomita kama 3.2. Hivyo tutakuwa tumeunganisha barabara yote kwa kiwango cha lami. Ni kumsisitiza tu meneja amsimamie mkandarasi kwa ukaribu. Ahsante.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa upembuzi yakinifu nimekuwa nikijibiwa kila mara kwamba utakamilika. Upembuzi huu ni kwaajili ya barabara kutoka Kahama – Nyangh’wale – Busisi. Je, ni lini upembuzi huo utakamilika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, barabara hii ni ndefu na upembuzi unaendelea kadiri muda unavyokwenda, ni kwamba tu hatuwezi tukaruka hatua. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakamilisha upembuzi na baada ya hapo hatua zitakazofuata itakuwa ni kutafuta fedha kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, Barabara ya Bugene, Nkwenda mpaka Isingiro inasababisha ajali kwa sababu ya vumbi kubwa; Je, ni lini ujenzi wake utaanza? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante; labda tu cha kwanza ni kuhakikisha kwamba kama kuna vumbi ndiyo barabara zilivyo za vumbi, lakini Serikali imeendelea kutafuta fedha kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Pakiwa ni barabara ya vumbi haiepukiki, lakini Serikali inaendelea kutafuta fedha kuzijenga hizo barabara kwa kiwango cha lami ikiwa ni pamoja na kupunguza ajali kwenye maeneo husika. Ahsante.

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tukuyu Mjini kuna barabara ya lami inayojengwa kule njia ya kwenda Masoko, tunashukuru. Barabara ile mkandarasi ameweka kifusi kikubwa maeneo ya Ranbos kuelekea Mpindo; sasa, je, ni lini mkandarasi yule atasawazisha kifusi hicho ili wananchi wa Mpindo wapite vizuri? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, haya ni maelekezo tu kumuelekeza; namuelekeza Meneja wa Mkoa wa Mbeya wa TANROADS kuhakikisha kwamba anamsimamia mkandarasi huyo kuondoa kifusi na kukisawazisha haraka inavyowezekana. Ahsante.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, barabara ya Kamanga – Sengerema imetangazwa kwa ajili ya ujenzi wa lami;

Je, ni lini mkandarasi atakuwa site kwa ajili ya kuanza kazi ya ujenzi wa Barabara ya Kamanga – Sengerema?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa barabara hiyo ni kwa mwaka huu kwa hiyo taratibu zinaendelea, zikishakamilika barabara hiyo itatangazwa kuanza kujengwa, ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 10

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ni miezi mitatu sasa Barabara ya Masasi – Nachingwea mkataba ulisainiwa;

Je, ni lini ujenzi wake utaanza? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara kama nimemsikia Masasi – Nachingwea – Liwale ni barabara ambazo ziko kwenye EPC+F na taratibu za kuzijenga hizi barabara zote zinaendelea, ikiwa ni pamoja na kuangalia maeneo ya kujenga makambi, kuvigawa vipande ambavyo vitatumika kujenga hizo barabara lakini pia mkandarasi kupitia upya usanifu na kuangalia fidia ambazo zitalipwa kwa wananchi ambao wataathirika na ujenzi. Kwa hiyo taratibu zimeshaanza na zinaendelea. Ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 11

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante; Barabara ya Mugakorongo – Kigalama mpaka Mrongo mkandarasi alishapatikana; ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara ambazo zilitangazwa kwamba zitakuwa zimesainiwa, barabara anayoisema tayari mkandarasi alishapatikana na taratibu zinafanyika kwa ajili ya barabara hiyo, kuanzia upande wa Mrongo. Tunachosubiri sasa hivi ni kufanya signing na kumkabidhi mkandarasi site ili aanze kijenga. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 12

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; Barabara ya kutoka Namtumbo – Mtonya – Mgombasi kuna daraja linalohatarisha usalama wa watu na mali zao;

Je, ni lini daraja hilo sasa litakarabatiwa katika Mto Luwegu? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, nimuagize Meneja wa Mkoa wa Ruvuma kwenda kulitembelea hilo daraja; na kama daraja hilo halijatengewa fedha za matengenezo aweze kuleta tathmini ili tuondokane ama tusije tukapata ajali. Atuletee Wizarani gharama na tuweze kulikarabati daraja hilo. (Makofi)