Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 6 2023-08-29

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, ni lini barabara ya Gairo hadi Nongwe itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Gairo – Labeho hadi Nongwe yenye urefu wa kilomita 54.06 kwa kiwango cha lami baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Tayari maandalizi ya nyaraka za zabuni yamekamilika na zabuni kwa ajili ya kumpata mhandisi mshauri wa kufanya usanifu zitatangazwa mwezi Septemba, mwaka huu 2023 na zitafunguliwa mwezi Oktoba, 2023. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, ahsante.