Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, ni fursa gani za uwekezaji zinapatikana Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ni bahati kubwa kuuliza swali la kwanza kabisa kwenye Wizara mpya ya Mipango na Uwekezaji.

Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Serikali imefanya utafiti gani mpya na upembuzi wa kina kufahamu fursa mpya za uwekezaji zinazoendana na sayansi na teknolojia? Kama imefanya hivyo, je ni kwa nini sasa Serikali isione umuhimu wa kuweka taarifa hizi zinazoendana na wakati kwenye tovuti za Wizara zinazotangaza masuala ya uwekezaji? Kwa sababu hata hao wawekezaji wanaangalia kwenye tovuti hizo. (Makofi)

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nusrat Hanje, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Kituo cha Uwekezaji kila mwezi inatoa taarifa mpya ambayo inaonyesha fursa ambazo zimejitokeza. Pia inatoa taarifa kuhusu aina ya uwekezaji ambao umefanyika katika mwezi huo lakini tupokee ushauri wake kuhusu kuweka kwenye website ya Wizara. Nimtaarifu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ndio kwanza ofisi hii imeanzishwa na tupo katika mchakato wa kuanzisha taasisi mbalimbali ikiwemo suala la website, ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - Je, ni fursa gani za uwekezaji zinapatikana Tanzania?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kulingana na fursa mbalimbali ambazo Mheshimiwa Waziri ameziainisha hapa zimepelekea kuwepo kwa wimbi kubwa la wawekezaji kutaka kuja kuwekeza nchini. Sasa nilitaka kujua, je, Serikali inatumia vigezo vipi kuweza kuwatambua wawekezaji wenye tija kwa Taifa hili? (Makofi)

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Nchi yetu kwa sasa inapokea idadi kubwa ya wawekezaji na tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa mazingira mazuri ambayo anayaweka katika kuvutia wawekezaji. Lakini tunavyo vigezo maalum vingi vya kuweza kutambua ni mwekezaji gani tumpokee na tumpeleke wapi. Naomba nitaje vitano tu;

(i) Tunahakikisha kwamba tunapokea uwekezaji ambao hatimaye utasababisha kukidhi mahitaji ya bidhaa za ndani;

(ii) Tunapendelea sana uwekezaji ambao hatimaye utaongeza thamani ili kuhakikisha kwamba tunaongeza thamani ya vitu vyetu ikiwepo kwenye thamani ya mazao;

(iii) Tunaangalia uwekezaji ambao hatimaye utazalisha ajira kwa watu wetu. (Makofi)

(iv) Tunazingatia sana uwekezaji ambao utatusaidia kuongeza mauzo ya bidhaa nje ya nchi ili kuongeza fedha za kigeni na;

(v) Tunazingatia sana uwekezaji ambao utadhalisha utajiri kwa watu wetu kwa hivyo kuchochea uwekezaji ndani.

Mheshimiwa Spika, hayo ni baadhi ya vigezo ambavyo tunazingatia.