Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali kuhusu kadhia ya maji yanayotuama maeneo mengi wakati wa mvua katika Jiji la Dar es Salaam?

Supplementary Question 1

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, kwanza niseme sijaridhika na jibu la Serikali.

Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; hivi Serikali ina mkakati gani haswa wa kuwatumia ma- engineer waliobobea, ma-engineer wa TANROADS, ma-engineer wa TARURA kufanya kazi ya kutatua hili tatizo ambalo ni kubwa sana kwa nchi?

Mheshimiwa Spika, pili; pesa zilizotumika ni nyingi mno kujenga barabara Mkoa wa Dar es Salaam, kujenga barabara kutoka airport kuja Dar es Salaam lakini maji yanayotuama yanaharibu kabisa sura ya Dar es Salaam. Serikali mnatuambia nini leo kitu cha uhakika? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mama yangu, Mheshimiwa Anne Kilango Malecela kwamba Serikali kwa kiasi kikubwa ukiangalia kasi ya mafuriko ya barabarani; kwa mfano nenda Tandale, nenda Sinza, nenda maeneo mengi ya Kigogo, Waheshimiwa Wabunge wa Dar es Salaam ni mashahidi, siku za nyuma kulikuwa na mafuriko mengi sana kulikuwa hakukaliki lakini kwa sasa kuna improvement kubwa sana baada ya Mradi wa DMDP na kazi hii inaendelea.

Mheshimiwa Spika, sasa kuhusiana na mkakati wa kuwatumia ma-engineer wabobevu wa TANROADS na TARURA hicho ndicho ambacho Serikali inafanya. Kabla ya ujezi wa mifereji na kingo za mito, engineer hawa wabobevu wanafanya tathmini na kutengeneza ramani na michoro na kazi hizi zinafanyika.

Mheshimiwa Spika, pia, ni kweli bado kuna changamoto kwenye barabara zetu za Jiji la Dar es Salaam kujaa maji mvua zikinyesha na ni suala endelevu ambalo inatakiwa Serikali iendelee kutenga fedha na kuendelea kwa hatua ya kujenga. Nimuhakikishie Mheshimiwa Kilango Malecela kwamba Serikali itaendelea kufanya kazi hiyo, ahsante.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali kuhusu kadhia ya maji yanayotuama maeneo mengi wakati wa mvua katika Jiji la Dar es Salaam?

Supplementary Question 2

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwa mujibu wa swali hili ni kwamba maji pia hutuama katika barabara za lami ambazo nyingi zinakuwa na mashimo na hata zikitengenezwa mashimo yanajirudia pale pale.

Je, Serikali haioni kwamba sasa ni muhimu kuwa na kitengo katika moja ya halmashauri za Jiji za Dar es Salaam kusimamia utengenezaji wa mashimo yale badala ya kutegemea kandarasi ambazo zikifanya kazi bado mashimo yanatokea tena? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Abbas Tarimba, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina kitengo tayari cha usimamizi wa matengenezo ya mara kwa mara ya barabara zetu, yakiwemo haya mashimo ambayo yanasababisha maji kutuama. Vitengo hivyo ni Idara za Wakuu wa Idara, kwanza tuna TARURA kila halmashauri ya wilaya, pia tuna ngazi ya mkoa lakini pia kwenye halmashauri kuna ma-engineer. Kwa hiyo, wale ndio wataalamu na vitengo vile ni sahihi kusimamia.

Mheshimiwa Spika, kinachokosekana mara nyingine ni uthabiti na umakini wa usimamizi kwa vile vitengo ambavyo vina ma-engineer tayari. Sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutaendelea kusimamia kwa karibu na kuchukua hatua kwa wale ma-engineer ambao hawatimizi majukumu yao ipasavyo, ahsante.