Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 4 2023-08-29

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali kuhusu kadhia ya maji yanayotuama maeneo mengi wakati wa mvua katika Jiji la Dar es Salaam?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Jimbo la Same Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za kudhibiti athari zinazotokana na mvua katika Jiji la Dar es Salaam; ikiwemo kujenga kingo za mito na mifereji mikubwa yenye urefu wa kilomita 30.7 kwa thamani ya shilingi bilioni 60 kupitia Mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam (DMDP).

Mheshimiwa Spika, kupitia Mradi wa DMDP awamu ya pili, Serikali inafanya usanifu na utambuzi wa maeneo kwa ajili ya ujenzi wa mifereji na mito yenye urefu wa kilomita 101.15, inayokadiriwa kutumia shilingi bilioni 200 katika wilaya zote za Mkoa wa Dar es Saalaam.

Mheshimiwa Spika, vilevile, TARURA kwa kushirikiana na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) wanaendelea na ukamilishaji wa kazi ya ununuzi kwa ajili ya uboreshaji wa Mto Msimbazi, ikiwa ni jitihada za Serikali kuendelea kukabiliana na mafuriko katika Jiji la Dar es Salaam, ahsante.