Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga soko na stendi ya kisasa eneo la Njiapanda Merya Halmashauri ya Wilaya ya Singida?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Pamoja na majibu haya ya Serikali. Nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kwa kuwa soko hili pamoja na stendi ni hitaji kubwa la Wananchi wa Singida Kaskazini. Je, ni lini hasa Serikali itakamilisha hiyo tathmini ili kuweza sasa kutoa nafasi kwa miradi hii kuanza kutekelezeka? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa halmashauri imeanza kutenga fedha kidogo kidogo lakini hazitoshi. Je, Serikali sasa ina mkakati gani mahsusi ya kuhakikisha inatumia vyanzo vingine vya fedha kuhakikisha ina supplement ili kukamilisha miradi hii kwa wakati? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhani, Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba soko na stendi hii ni hitaji kubwa la wananchi na Serikali inatambua hili na ndio maana imeelekeza ifanyike tathmini. Tumewaalekeza Halmashauri hii ya Singida ihakikishe inakamilisha tathmini ndani ya miezi mitatu na kuleta maandiko hayo Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili yaweze kupitiwa na kufanyiwa maamuzi.

Mheshimiwa Spika, pili, Serikali itatenga fedha baada ya kufanya tathmini, itatenga fedha kwa ajili ya kuongeza nguvu za kukamilisha ujenzi wa stendi lakini pia soko ambalo linahitajika, ahsante.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga soko na stendi ya kisasa eneo la Njiapanda Merya Halmashauri ya Wilaya ya Singida?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba kufahamu ni lini Serikali itatujengea soko pamoja na Stendi ya Mkoa wa Songwe? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Juliana Shonza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba Mkoa wa Songwe ni miongoni mwa mikoa mipya, hauna stendi lakini na soko na suala hili limekuwa likiulizwa mara kwa mara na Serikali imeendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa stendi na soko katika Mkoa wa Songwe. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ipo kazini na itatekeleza suala hilo, ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga soko na stendi ya kisasa eneo la Njiapanda Merya Halmashauri ya Wilaya ya Singida?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga Soko la Haydom na stendi yake na bahati nzuri Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tulielekeza Halmashauri ya Mbulu Vijijini kufanya tathmini na kuanza kutenga fedha za mapato ya ndani kwa awamu kwa ajili ya ujenzi wa Soko la Haydom. Kwa hiyo, nitumie fursa hii kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kusisitiza maelekezo hayo yafanyiwe kazi na pale itakapohitajika nguvu ya Serikali Kuu basi tutakwenda kuunga mkono juhudi za ujenzi wa soko hilo, ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga soko na stendi ya kisasa eneo la Njiapanda Merya Halmashauri ya Wilaya ya Singida?

Supplementary Question 4

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona, je, ni lini Mradi wa TACTIC utaanza ili soko na stendi vijengwe Bukoba Mjini? Hili swali nimeshaliuliza zaidi ya mara tatu ndani ya Bunge hili, ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Oliver Semuguruka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimtoe shaka Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeanza utekelezaji wa Mradi wa TACTIC kwa awamu ya kwanza lakini awamu ya pili pia tathmini zinaendelea na awamu ya tatu itakwenda kutekelezwa. Kwa hiyo, Halmashauri ya Bukoba pia ipo katika moja ya awamu hizi na mradi huu utatekelezwa, ahsante. (Makofi)