Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2023-08-29

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga soko na stendi ya kisasa eneo la Njiapanda Merya Halmashauri ya Wilaya ya Singida?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abeid Ighondo Ramadhani, Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida imeanza utekelezaji wa hatua za awali za ujenzi wa Stendi ya Njiapanda ya Merya. Katika mwaka wa fedha 2019/2020 halmashauri ilitenga kiasi cha shilingi milioni 10 na kufanya upimaji wa eneo la stendi, kufanya usafi na kusawazisha eneo.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali inakamilisha tathmini ya gharama za ujenzi wa stendi hiyo na kuanza kutenga bajeti katika mwaka wa fedha 2024/2025 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi. Halmashauri inaendelea na maandalizi ya andiko la mradi wa soko na litakapokamilika litawasilishwa Serikalini kwa ajili ya uchambuzi na endapo litakidhi vigezo litatengewa bajeti na kuanza ujenzi, ahsante.