Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza: Kwa kuwa kituo hicho cha Kizazi kilianza kujengwa kwa nguvu za wananchi tangu 2019, mpaka sasa ni miaka mitano; na ninaishukuru Serikali kwa kutenga fedha hizo, lakini mpaka sasa hazijaanza kwenda; nataka Serikali inihakikishie: Je, ni lini kituo hicho kitakamilika ili wananchi waanze kupata huduma katika kituo hicho? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Katika Halmashauri ya Kasulu DC, ipo zahanati katika Kata ya Kagerankanda, zahanati ya Uvinza ina watumishi wawili tu, tena wanaume: Je, ni lini Serikali itamwagiza Mganga Mkuu pamoja na Mkurugenzi kupeleka watumishi wa kile katika zahanati hiyo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niitumie fursa hii kuwapongeza wananchi wa Kibondo kwa kuchangia nguvu zao katika ujenzi wa kituo cha afya na ndiyo maana Serikali imetambua nguvu zao na kuweza kutenga shilingi milioni 500 ambayo itapelekwa ndani ya mwaka huu wa fedha; na mara baada ya fedha hizo kupelekwa, tunawapa maelekezo ya ndani ya miezi sita kituo cha afya kiwe kimekamilika, wananchi waanze kupata huduma za afya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, kuhusu Zahanati ya Uvinza katika Halmashauri ya Kasulu DC ambayo ina watumishi wawili wa kiume, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumelichukua hilo, tutalifanyia kazi, lakini Serikali imeendelea kuajiri watumishi. Niseme, katika kipindi cha miaka miwili cha uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan watumishi wa afya 17,000 wameajiriwa na kupelekwa kwenye vituo vyetu na zoezi hilo litaendelea kwa kadri ya upatikanaji wa fedha, ahsante.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa kujenga vituo vingi vya afya katika mkoa wangu wa Arusha na vyenye ubora wa hali ya juu, lakini changamoto kubwa ni vifaa tiba ikiwemo na kichomeataka hali inayopelekea akina mama wengi kukosa huduma ya kujifungua: Nini kauli ya Serikali?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, napokea pongezi hizi za kazi nzuri ya Serikali. Nimhakikishie kwamba fedha za ununuzi wa vifaa tiba zimeendelea kutolewa na vifaa tiba vimesambazwa kwenye vituo, na pia mwaka huu wa fedha fedha zimetengwa kwa ajili ya vifaa tiba. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba zahanati hii itapewa kipaumbele pamoja na ujenzi wa incinerator, ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kituo cha Afya cha Makorongo kimeanza kutumika, lakini baadhi ya majengo hayajakamilika. Mfano, jengo la maabara. Nini kauli ya Serikali ya kukamilisha ujenzi huu? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kituo kile kimeanza kutoa huduma za afya lakini jengo la maabara na baadhi ya majengo hayajakamilika na ujenzi huu tunakwenda kwa awamu. Nikuhakikishie kwamba Serikali inatafuta fedha kupitia mapato ya ndani lakini pia kupitia Serikali kuu ili kukamilisha majengo haya, kituo kiweze kutoa huduma vizuri zaidi, ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?

Supplementary Question 4

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kituo cha Afya cha Nobola kilichopo katika Tarafa ya Negezi, kimejengwa miaka mingi miaka ya 1970 na kituo hiki kimechakaa sana: Nini mpango wa Serikali wa kukarabati kituo hiki ikiwa ni pamoja na kufanya upanuzi kwa ajili ya kituo hiki? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Butondo, Mbunge wa Jimbo la Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya vituo vyote vya afya, hospitali kongwe na kuweka mpango kazi wa ukarabati kila mwaka wa fedha. Ndiyo maana katika mwaka huu wa fedha pia katika bajeti yetu tuna fedha kwa ajili ya ukarabati wa vituo hivi vikongwe. Kwa hiyo, nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaelekeza Halmashauri ya Kishapu kuleta taarifa ili timu iweze kufanya tathmini na kuona mahitaji ya ukarabati na upanuzi wa kituo hicho, ahsante.

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?

Supplementary Question 5

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, Serikali iko tayari kujua sababu za kwa nini Kituo cha Afya cha Iramba Ndogo hakijakamilika ili kiweze kuchukua hatua na kunufaisha wananchi kama ilivyokusudiwa? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Leah Komanya, Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali iko tayari kufanya tathmini na kujua sababu zilizopelekea kituo hiki cha afya kutokamilika. Pia itachukua hatua za kisheria na za kinidhamu ikithibitika kuna baadhi ya watumishi ambao hawakufuata taratibu za fedha na kusababisha kituo kutokamilika, ahsante.

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?

Supplementary Question 6

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kituo cha Afya cha Kata ya Ifumbo ni kituo cha afya cha muda mrefu na kinajengwa kupitia mapato ya ndani ya halmashauri. Je, ni lini Serikali itatoa fedha ya kituo hiki kiweze kukamilika na Wananchi wa Ifumbo waweze kunufaika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masache Kasaka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina utaratibu wa ujenzi wa vituo vya afya kwa kutumia nguvu za wananchi. Niwapongeze Wananchi wa Kituo cha Afya cha Ifumbo lakini tunaendelea kusisitiza kwamba kupitia mapato ya ndani watenge ile asilimia 20, 40 na 60 kwa ajili ya kukamilisha vituo hivi. Endapo halmashauri haina uwezo huo walete andiko hilo ili Serikali iweze kuchangia fedha kwa ajili ya kukamilisha kituo hicho, ahsante.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?

Supplementary Question 7

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru. Kata ya Kakola kwenye Jimbo la Tabora Mjini ina jengo la mama na mtoto kwenye zahanati yao. Serikali ina mpango gani wa kumalizia boma hili ili kunusuru afya ya mama na mtoto katika Manispaa ya Tabora? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hawa Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kumuelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kutenga fedha kwa ajili ya kukamilsha boma hili ambalo Mheshimiwa Mbunge amekuwa mara kwa mara analifuatilia. Fedha inayohitajika ni kidogo iko ndani ya uwezo wa halmashauri na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutafuatilia, ahsante. (Makofi)

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Kizazi – Kibondo?

Supplementary Question 8

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Wananchi wa Vijiji wa Mganzi, Chagana, Nguvumoja, Ilogelo na Mwagala, Jimbo la Igunga wamekamilisha ujenzi wa maboma ya zahanati; je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi kuunga nguvu za wananchi mkono? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nicholaus Ngassa, Mbunge wa Jimbo la Igunga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ukamilishaji wa maboma ya zahanati yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi lakini ukamilishaji unaenda kwa awamu. Tumeshafanya katika miaka miwili, mitatu yote ya fedha na tutaendelea kufanya hivyo kwa kutumia fedha za mapato ya ndani lakini pia kutumia fedha za Serikali Kuu, ahsante.