Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza eneo na kuboresha Skimu ya Umwagiliaji ya Mto Ruvu – Bagamoyo?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nina maswali mawili ya nyongeza. Bonde la Mto Ruvu katika sehemu ya Bagamoyo lina wakulima wengi sana ambao wanatokea Kata za Yombo, Magomeni na Makurunge: Je, ni lini sasa Serikali itawaombea wananchi hawa kupata eneo la Magereza ambalo ni kubwa na halina kazi yoyote inayoendelea ili waweze kufanya kilimo na kupata mahitaji yao?

Swali la pili. Mheshimiwa Waziri ni lini atakuja Bagamoyo kutembelea skimu ya umwagiliaji Ruvu inayojulikana maarufu kama JICA ili kuweza kuja kuzungumza na wakulima pale na kutupa matumaini kwa ajili ya kutengeneza skimu ile? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli pale kwenye eneo la Gereza la Kigongoni tunazo hekta zaidi ya 1,350 na kumekuwa na changamoto juu ya matumizi ya wananchi katika ardhi ya eneo hilo. Nachukua fursa hii kumwagiza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji waende kukaa na uongozi wa gereza ili waone namna ambavyo wananchi wa kata ulizozitaja wataweza kushiriki kilimo katika eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili la kuhusu kutembelea Bagamoyo baada tu ya vikao vya Bunge la Bajeti, mimi na wewe tutakwenda kuzungumza na wakulima ili tuweze kusikiliza changamoto zao na tuweze kuwatatulia ili wafanye kilimo cha umwagiliaji.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza eneo na kuboresha Skimu ya Umwagiliaji ya Mto Ruvu – Bagamoyo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Je, ni lini skimu ya umwagiliaji ya Kwamtonga iliyopo kwenye Kata ya Sungaji Wilayani Mvomero itafanyiwa uboreshaji kusudi wananchi wengi waweze kulima kwa mwaka mzima kwani maji ya kutosha yapo? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kiambatanisho Na. 8 katika bajeti ya Wizara ya Kilimo aliyosoma Mheshimiwa Waziri, tumeorodhesha skimu zote ambazo tutazifanyia ukarabati na ikiwemo skimu ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja. Nimwondoe hofu, hii kazi itafanyika.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza eneo na kuboresha Skimu ya Umwagiliaji ya Mto Ruvu – Bagamoyo?

Supplementary Question 3

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Skimu ya Umwagiliaji ya Ndungu, Jimboni Same Mashariki, imepoteza ubora wake kabisa. Ni skimu ambayo wananchi wanaitegemea sana katika Tarafa ya Ndungu: Je, Mheshimiwa Waziri ni lini utakuja kuiona ili uone pamoja na Mto Saseni? Vipo karibu.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ahadi ya Serikali kupitia Bunge lako Tukufu ambayo tuliitoa humu ndani kwamba tutakwenda kuzitembelea skimu hizo, lakini kabla sijafanya hivyo, nitamwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Umwagiliaji pamoja na wataalam wake wapite kwanza kuangalia, nami na Mheshimiwa Mbunge tutaongozana pamoja kwenda kuzungumza na wananchi na kutatua kero ambazo wananchi wanazo katika eneo hilo.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza eneo na kuboresha Skimu ya Umwagiliaji ya Mto Ruvu – Bagamoyo?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Wananchi wa Ushetu wametenga hekta zaidi ya 5,000 ambazo ni nzuri na zina mtiririko wa maji kwa ajili ya umwagilijaji: Serikali inakuja lini kuwajengea skimu ya umwagiliaji wananchi wa Jimbo la Ushetu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwapongeze Halmashauri kwa kutenga eneo kubwa hilo kwa ajili ya umwagiliaji. Maelekezo yangu ni kumwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kupeleka wataalam kwenda kuliangalia eneo hilo kama linafaa kwa ajili ya kuweka miundombinu basi, Serikali itahakikisha kwamba inaweka miundombinu katika eneo hilo. (Makofi)

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza eneo na kuboresha Skimu ya Umwagiliaji ya Mto Ruvu – Bagamoyo?

Supplementary Question 5

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kata ya Litumbandyosi tulipata skimu katika bajeti hii. Ni lini sasa skimu hii inaenda kuanza ujenzi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bonde la Litumbandyosi ni kati ya mabonde 22 ambayo tarehe 20 mwezi wa tatu mwaka huu tulisaini mkataba na wakandarasi kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kazi hii inaendelea. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hii inakamilika mwaka wa fedha huu ambao unaishia. Kuanzia Julai kazi itaanza ili kuwafanya wananchi wako waweze kufanya Kilimo cha Umwagiliaji.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza: - Je, lini Serikali itaongeza eneo na kuboresha Skimu ya Umwagiliaji ya Mto Ruvu – Bagamoyo?

Supplementary Question 6

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Halmashauri ya Mji wa Bunda inazungukwa na Ziwa Victoria na hatuna uhaba kabisa wa maeneo. Je, Mheshimiwa Waziri, ni lini mtatujengea skimu ya umwagiliaji ikiwa ni moja ya mkakati wa kuhamasisha vijana kujihusisha na kilimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti yetu tumeeleza vizuri kabisa, maeneo yote ambayo yana vyanzo vya uhakika vya maji hasa ikiwemo mito na maziwa tutahakikisha tunawawezesha wakulima wa maeneo hayo kufanya kilimo kupitia umwagiliaji. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge juu ya eneo lake la Bunda, pia tutafanya kazi hiyo kuhakikisha kwamba wakulima wa Bunda wanafanya kilimo cha umwagiliaji.