Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, kwa nini ukomo wa saa za kufundisha Wanafunzi haujawekwa kisheria kama ilivyowekwa kwa saa za kazi kwa Waajiriwa?

Supplementary Question 1

MHE. NG'WASI D. KAMANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Tunatambua kwamba lengo la Serikali kuweka utaratibu huu ni pamoja na kutambua uwezo wa kiakili wa watoto wetu pamoja na uwezo wao wa kusoma kwa muda fulani. Tunavyozungumza, kuna shule za primary hasa za watu binafsi ambazo mwanafunzi wa kutwa anaenda shuleni kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja na wa bweni anasoma tena kuanzia saa moja mpaka saa tatu au saa nne usiku, zaidi ya muda ambao umepangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Je, Serikali inatambua kwamba kuna shule ambazo zinafanya utaratibu huu ambao ni kinyume kabisa na utaratibu na inahatarisha afya za akili za watoto wetu? Kama inatambua, inachukua hatua gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa ajili ya umuhimu wa afya za akili za watoto wetu: Je, Serikali haioni haja kwenye marekebisho haya yanayofanyika ya utaratibu wa elimu na mfumo wake kuliingiza suala hili katika mfumo? Ahsante.

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kwa pamoja ya Mheshimiwa Ng’wasi Damas Kamani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kwamba ziko shule ambazo wanafunzi wanakaa muda mrefu zaidi shuleni na vile vile wanatumia muda mrefu sana kwenda shuleni na kuna aina mbili ya changamoto katika jambo hili. Kwanza, sio wanafunzi wote wanatumia mitaala ile ile. Ziko shule ambazo zinatumia mitaala tofauti na ile ambayo imetolewa na Serikali. Kwa mfano, kuna wale wanaotumia mitaala ya Cambridge na muda wao wa kusoma siyo lazima uwe sawa na muda wetu. Pili, kwa kuchagua shule, hasa hizi binafsi na umbali wa shule na nyumbani, baadhi ya wanafunzi wanajikuta wanaondoka mapema sana nyumbani na wanarudi kwa kuchelewa sana, kwa sababu tu ya choice ya wazazi kwamba pengine wanaishi Mbezi Beach lakini mtoto wako anaenda kusoma Kimara tofauti na kusoma eneo lile lile la Mbezi Beach.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili suala ni changamoto kweli kwa sababu tungependa watoto wapate fursa vile vile ya kucheza na kuwa watoto na kuwa na makuzi mazuri na wasitumie muda wote tu kwa ajili ya shughuli za darasani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutajitahidi kuendelea kukaa na wadau wa shule binafsi kuangalia namna bora zaidi ya kutatua changamoto hii. Vile vile tunaendelea kuhimiza ujenzi wa shule mbalimbali za watu binafsi ziwe karibu zaidi na makazi ya watu na kuhimiza wazazi wachague shule ambazo ziko karibu zaidi na nyumbani ili watoto wasitumie muda mrefu sana barabarani wakati wanaenda shuleni.

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, kwa nini ukomo wa saa za kufundisha Wanafunzi haujawekwa kisheria kama ilivyowekwa kwa saa za kazi kwa Waajiriwa?

Supplementary Question 2

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Shule ya Msingi Bupandwa, Kasisa, Ruhama, Mwabasabi zina uhaba mkubwa sana wa walimu na hivyo kuwafanya walimu kufundisha kwa masaa mengi kuliko kawaida na watoto kushindwa kuelewa: Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuwasiliana na Waziri wa TAMISEMI ili aweze kututafutia walimu wa kutosha watoto wetu waweze kujifunza kwa urahisi na kuelewa?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shigongo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna maeneo yana uhaba mkubwa wa walimu, mtawanyiko wa walimu siyo sawia kama ambavyo tungependa. Bahati nzuri kuna nyongeza, walimu wataajiriwa hivi karibuni na tunazungumza na wenzetu wa TAMISEMI ili kuhakikisha kwamba walimu wale wanatawanywa maeneo yale ambayo yana uhitaji mkubwa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, sasa hivi tuna utaratibu wa kuweza kutumia walimu wa kujitolea kwa ajili ya kuendelea kupunguza uhaba wa walimu na tutaendelea na jitihada hizi ili kuhakikisha kwamba kweli wanafunzi wote popote pale Tanzania wanapata huduma ya kufundishwa kama inavyotakiwa.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: - Je, kwa nini ukomo wa saa za kufundisha Wanafunzi haujawekwa kisheria kama ilivyowekwa kwa saa za kazi kwa Waajiriwa?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tunatambua na tunajua kwamba elimu ni haki ya msingi kwa mtoto na kwa mwanadamu; na amesema kwamba kuna ile ratiba ambayo imepangwa elimu ya awali, elimu ya msingi mpaka elimu ya Sekondari; sambamba na hilo, kuna suala zima la watoto wenye mahitaji maalum hasa autism: Je, ratiba hii inaenda sambamba na hayo ambayo Mheshimiwa Waziri ameyasema?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tuna wanafunzi wenye mahitaji maalum na ambao wanahitaji muda mrefu zaidi kusoma kwa ajili ya kuweza kulingana na wenzao darasani. Njia mojawapo ambayo inatumika sasa hivi wakati wa kufanya mitihani kulingana na changamoto ambayo inafahamika, wanafunzi wanapewa muda tofauti wa kufanya mitihani. Vile vile katika mitaala mipya hii, hili suala limeangaliwa kutokana na maoni ya wadau ili kuhakikisha kwamba kweli tunatoa unyumbufu wa kutosha kuweza kuwa-commodate wale wanafunzi wenye mahitaji maalum hasa wakati wa kufundisha darasani.