Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 413 2023-05-23

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NG'WASI D. KAMANI aliuliza: -

Je, kwa nini ukomo wa saa za kufundisha Wanafunzi haujawekwa kisheria kama ilivyowekwa kwa saa za kazi kwa Waajiriwa?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ng’wasi Damasi Kamani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Elimu haijaweka ukomo wa saa za kufundisha wanafunzi ili kutoa fursa ya mtaala kuwa nyumbufu kulingana na mahitaji maalumu ya ujifunzaji wa wanafunzi wote pamoja na mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mitaala ya Elimu ya Msingi na Sekondari imeweka bayana Muda (duration) unaopaswa wanafunzi kusoma. Mtaala wa Elimu ya Msingi unaeleza kuwa muda wa kusoma Elimu ya Awali na Darasa la I - II ni masaa matatu tu kwa siku na kipindi kimoja ni dakika 30. Aidha, Muda wa kusoma kwa darasa III - VII ni masaa sita kwa siku na kila kipindi ni dakika 40. Aidha, kwa upande wa Elimu ya Sekondari muda wa kusoma ni masaa matano na dakika 20 na kipindi kimoja ni dakika 40. Aidha, kwa mwaka wanafunzi hutakiwa kusoma kwa siku 194.