Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: - Je Serikali inachukua hatua gani za kimkakati kufikia usawa wa kijinsia 50/50 ifikapo 2025?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na mikakati hiyo mizuri ya Serikali, wanawake wa Tanzania wanataka kusikia: Je, ifikapo mwaka 2025 asilimia hii 50 kwa 50 itakuwa imefikiwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Hivi sasa tumeshuhudia jinsi wanawake waliopo kwenye nafasi mbalimbali wanavyofanya kazi kwa weledi na ufanisi mkubwa. Kwa mfano tu, Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Spika wetu, Mheshimiwa Dkt. Tulia: Je, Serikali ina mikakati gani sasa ya kuwainua kiuongozi wanawake hasa kwenye ngazi ya chini ili basi wainuke kiongozi? Ahsante.

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna. Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ni mtekelezaji mzuri wa ilani. Katika kipindi chake cha miaka miwili ameshafikia asilimia 31 ya uteuzi wa wanawake viongozi. Kwa vile mamlaka ya uteuzi ni yake, tuendelee kumwamini katika majukumu yake na kufikia 50 kwa 50. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, Serikali imeridhia na inatekeleza mikataba ya Kimataifa na kikanda kuhusu usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake, lengo ni kukuza ushiriki wa wanawake katika nyanja zote za maendeleo ikiwemo kuhakikisha usawa katika ngazi nyeti na nafasi nyeti za uongozi na maamuzi nchini, ahsante. (Makofi)