Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 412 2023-05-23

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI K.n.y. MHE. HUSNA J. SEKIBOKO aliuliza: -

Je Serikali inachukua hatua gani za kimkakati kufikia usawa wa kijinsia 50/50 ifikapo 2025?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Husna Juma Sekiboko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuundwa kwa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kama chombo maalum cha kuratibu ajenda ya kufikia usawa wa kijinsia. Aidha, hatua nyingine ni Serikali kuendelea kutoa fursa na nafasi za uongozi na maamuzi kwa wanawake mathalani, kipengele cha 12(4) cha Kanuni za Utumishi wa Umma mwaka 2013, kinasema, “Inapotokea mwanamke na mwanaume wametimiza vigezo sawa kwa kulingana, basi kipaumbele atapewa mwanamke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Sheria ya Serikali za Mitaa, Mamlaka za Miji na Wilaya ya Mwaka 1982, inasema kuwe na asilimia 25 ya ushiriki wa wanawake katika nafasi za uongozi na maamuzi. Aidha, katika uchaguzi wa mwaka 2000 na 2005 asilimia hizo zilipandishwa hadi kufikia asilimia 31 ambayo ni moja ya tatu ya ushiriki wa wanawake katika nafasi za uongozi na maamuzi, ahsante.