Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka maji katika Vijiji 62 Jimbo la Newala Vijijini ambavyo havina huduma ya maji?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini pia naishukuru Serikali kwamba kuna mradi mkubwa wa Makonde ambao wametupatia fedha unatekelezwa kwenye Wilaya yetu ya Newala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la msingi lilihusu Jimbo la Newala Vijijini. Kumbuka kwamba Newala ina Majimbo mawili ambayo ni Newala Mjini na Newala Vijijini, kwa hiyo swali lilikuwa specific kwa Newala Vijijini. Sasa kwa kujumlisha hivi tutashindwa kupata uhalisia wake wa tatizo hasa ni nini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi sasa, pamoja na yote yaliyojitokeza, kwenye Jimbo la Newala Vijijini kuna Mradi wa Maji wa Mnima – Miyuyu ambao umeanza kutekelezwa tangu mwaka 2018, na mradi ule ulikuwa ni wa miezi tisa. Mpaka sasa utekelezaji wake ni asilimia 65 tu. Pia changamoto ambayo inasababisha mradi huu kutokamilika ni kukosekana kwa fedha. Fedha zilizokuwa zimetengwa ni bilioni 1.3, zimelipwa milioni 614 tu. Je, ni lini Serikali itamaliza fedha zilizobakia ili wananchi wa Newala Vijijini waweze kupata maji?

Swali la pili, kwenye Vijiji vya Mkudumba, Mnyengachi, Mnyambe, Mnima, Bahati, Mikumbi, Mkongi, Namangudu, Nangujane, Chilende, Mkoma, ‘two’ pamoja na Lihanga kuna miradi ya maji ambayo inatekelezwa. Lakini miradi ile ina changamoto ya upatikanaji wa fedha.

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili miradi hii ikamilike? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Jimbo la Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa Miyuyu tatizo ni fedha na swali lake la pili tatizo pia ni fedha. Naomba niwe nimepokea masuala haya ya Newala Vijijini na nitafanyia kazi mimi mwenyewe kwa ukaribu kuhakikisha fedha zinakwenda na kazi inakamilika kwa wakati.

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka maji katika Vijiji 62 Jimbo la Newala Vijijini ambavyo havina huduma ya maji?

Supplementary Question 2

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa maeneo mengi katika Mkoa wa Lindi yana maji ya chumvi. Je, ni lini Serikali itawapatia maji safi na salama wananchi wa Kata za Ngunichile, Tarafa ya Kilimarondo na Namapwia kwenye Wilaya ya Nachingwea, Lihimalyao, Kibata na Kandawale kule Wilaya ya Kilwa? ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tecla kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo yote aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge ni kweli yana shida ya maji ya chumvi, Mheshimiwa Mbunge unafahamu mradi wetu mkubwa ambao tayari tumeongea, hata juzi tulikuwa pamoja na tayari tunautengea fedha ule mradi ili sasa tuweze kupata maji ya uhakika yakiwa safi na salama na kuondokana na visima hivi vinavyotuletea maji ya chumvi.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka maji katika Vijiji 62 Jimbo la Newala Vijijini ambavyo havina huduma ya maji?

Supplementary Question 3

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Katika kupunguza adha ya maji hususan Manispaa ya Ilemela, Serikali iliahidi kufufua visima vyote ambavyo havifanyi kazi. Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kufufua visima hivyo ili kuondokana na changamoto ya maji katika Manispaa ya Ilemela? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha Matondo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu visima kufufuliwa Ilemela, tayari tumeshaagiza na katika mwaka ujao wa fedha tutahakikisha visima hivi vyote ambavyo vimechimbwa na bado vina maji mazuri tutavitumia kuhakikisha vinaongeza huduma ya maji katika maeneo yote ya Ilemela. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka maji katika Vijiji 62 Jimbo la Newala Vijijini ambavyo havina huduma ya maji?

Supplementary Question 4

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Rais kwa kupeleka fedha, kiasi cha shilingi bilioni 138 kutoa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Rorya na Tarime. Nini kauli ya Serikali juu ya maji hayo kwenda katika Kata ya Komaswa, Manga, Nyamongo, Sirari, Pemba, Mbugi na Nyamwaga? Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Marwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi wa Ziwa Victoria wa kupeleka maji Rorya na Tarime, tayari usanifu unaendelea na Mheshimiwa Mbunge tumezungumza hapa juzi na nimekupa Katibu wangu amefanya kazi nzuri na wewe. Tutahakikisha mradi huu tunakuja kuutekeleza kwa wakati. (Makofi)