Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Water and Irrigation Wizara ya Maji 411 2023-05-23

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka maji katika Vijiji 62 Jimbo la Newala Vijijini ambavyo havina huduma ya maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Jimbo la Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Newala ina jumla ya vijiji 155 na kati yake vijiji 77 vinapata huduma ya maji. Serikali inaendelea na jitihada za kupeleka huduma ya maji kwenye vijiji visivyo na huduma na katika mwaka wa fedha 2022/2023 miradi 12 inaendelea kutekelezwa ukiwemo mradi mkubwa wa Makonde. Kukamilika kwa miradi hiyo kutanufaisha vijiji 61. Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itafanya usanifu wa miradi ya maji katika vijiji 17 vilivyobaki ikifuatiwa na utekelezaji.