Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, kwa nini Serikali haijazikarabati Meli za MV Liemba, MV Mwongozo na MV Sangara ambazo zimesimama kufanyakazi?

Supplementary Question 1

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kwanza nilitaka ifahamike kwamba meli ya MT Sangara ambayo imefikia asilimia 90.7 ni meli ya mafuta siyo ya abiria wala mizigo, inabeba mafuta tu na kwa maana hiyo haina msaada mkubwa kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa imekuwa kawaida kwa Serikali kila mwaka kutenga bajeti na kuleta hapa kwenye Bunge lakini hakuna utekelezaji, na kwa kuwa, katika Ziwa Tanganyika kwa sasa hakuna meli hata moja ya Serikali inayofanya kazi. Nataka commitment ya Serikali kwamba bajeti itapungua kwenye eneo lingine lolote la Wizara na siyo kwenye meli hii, kwamba lazima meli hizi zitatengenezwa na kurudi majini, nataka commitment ya Serikali. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana Mheshimiwa Waziri wetu wa Ujenzi na Uchukuzi amesoma bajeti ya Wizara yetu na ameonesha commitment ya kiwango cha juu kabisa kuhusiana na namna ambavyo Ziwa Tanganyika tunakwenda kujenga meli mbili mpya pamoja na chelezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi, commitment nyingine ya Serikali ni hizi meli ambazo hazifanyi kazi kwa sasa na tayari kwa mfano, hii MV Mwongozo ambayo tayari Mkandarasi ameshapatikana, ni Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) pamoja na hii meli ya MT Sangara ambayo amesema kweli ni ya mafuta lakini inafanya kazi katika Ziwa Tanganyika na iko asilimia 90. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote wa Mikoa ya Kigoma, Rukwa pamoja na Katavi, kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika mwaka wa fedha ujao inakwenda kufanya haya ambayo imeahidi hapa. Ahsante. (Makofi)