Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 410 2023-05-23

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali haijazikarabati Meli za MV Liemba, MV Mwongozo na MV Sangara ambazo zimesimama kufanyakazi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa kukarabati meli za MV. Liemba, MV Mwongozo na MV Sangara ili kuboresha huduma za usafiri kwa njia ya maji katika Ziwa Tanganyika. Ili kufikia azima hiyo, Serikali kupitia Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) inaendelea na ukarabati wa Meli ya MV Sangara ambapo kwa sasa kazi hiyo imefikia asilimia 90.7 na inatarajiwa kukamilika Septemba, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia MSCL ilikamilisha taratibu za zabuni kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa ukarabati wa meli ya MV Liemba tarehe 5 Machi, 2023 na kwa sasa MSCL inaendelea kufanya majadiliano na mkandarasi kabla ya kusaini mkataba. Mkataba wa ukarabati wa meli hiyo unatarajiwa kusainiwa Juni, 2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, kuhusu Meli ya MV Mwongozo ambayo ilisimamishwa kutokana na changamoto ya msawazo (stability), MSCL inakamilisha taratibu za kumwajiri Mhandisi Mshauri kwa ajili kufanya tathmini ya kina na kuishauri Serikali ipasavyo. Mhandisi Mshauri anatarajiwa kuanza kazi hii mwezi Juni na kukamilisha mwezi Novemba, 2023. Ahsante.