Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mlowo – Kamsamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Naibu Waziri, ninaomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza, ninataka nijue barabara hizo unganishi ambazo zimejengwa kwa kiwango cha lami ni zipi.

Swali langu la pili, barabara hii ya Mlowo – Kamsamba imekuwa na changamoto kubwa sana kwa wananchi wetu, lakini changamoto hizi zinatukosesha fursa muhimu za kiuchumi. Nataka kujua Serikali ina mkakati gani wa maksudi kuhakikisha inajenga barabara hizi kwa wakati na muda muafaka ili kuondoa changamoto ambazo wanakutana nazo wananchi wa Mkoa wa Songwe, Momba na maeneo mengine kwa ujumla. Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nimemuelewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichokuwa nasema tumeanza kuijenga, tuna Daraja la Mto Momba ambalo liko katika hiyo barabara, katika hilo daraja tumejenga approach roads ambazo zinaunganisha lile daraja ukitokea Mkoa wa Songwe na Mkoa wa Rukwa. Kwa hiyo, kwa pande zile mbili tayari kuna lami upande huu na huu, zile ndiyo barabara unganishi na lile daraja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la maksudi, kwamba je, tuna mkakati gani kuhakikisha kwamba tunajenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami. Bajeti inaendelea, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imetenga fedha, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, kwamba tutaanza kuijenga hiyo barabara ili kukuza uchumi pia kurahisisha usafiri kwa wananchi wa Mkoa wa Songwe wa Mlowo, Igamba, Utambalila, Kamsamba lakini pia Utambalila kwenda Makao Makuu ya Mji wa Momba ambayo ni Makao Makuu ya Wilaya. Ahsante.

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mlowo – Kamsamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi. Hii barabara ya Kibena – Lupembe – Madeke mpaka Morogoro ni barabara ya Kimkoa na ni kero ya muda mrefu ya wananchi wangu. Tarehe 19 Bungeni hapa Serikali iliahidi kuanza ujenzi wa kilometa 25 na sasa tuko kwenye bajeti ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi.

Naomba kauli ya Serikali barabara hii inaanza ujenzi lini? Ahsante.(Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge ni kweli ni barabara inayounganisha Mkoa wa Njombe na Mkoa wa Morogoro, pia yalitolewa maelekezo maalum na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwamba barabara hiyo ni lazima ianze kujengwa. Nami nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Jimbo la Lupembe kwamba katika bajeti hii tayari tumeshaanza taratibu za kuanza kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami, na tutaanza na kilometa 25 kwa kuanzia upande wa Mkoa wa Njombe, upande wa Morogoro tayari tuna kilometa 100 ambazo zinaendelea kujengwa na ziko kwenye taratibu za manunuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipande kilichobaki African Development Bank watakifanyia usanifu ili barabara yote iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mlowo – Kamsamba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimwia Mwenyekiti, Great Nyerere Road ni barabara muhimu sana kwa utalii wa Selous. Nimeona kwenye mapendekezo ya bajeti zimetengwa shilingi bilioni mbili ambayo ni sawa na kilometa mbili. Ni lini sasa Serikali itaanza kutenga fedha za kutosha ili tupate kilometa za kutosha kwa kuzingatia umuhimu wa barabara hii? ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa mpango wa bajeti kiasi tulichotenga aangalie kilometa ambazo tuna mpango wa kuzijenga. Ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara hii ya Kisarawe – Maneromango kwenda Hifadhi ya Taifa ya Nyerere yote inakamilika kwa kiwango cha lami. Ndiyo maana katika bajeti hii tumeshaweka fedha kuendelea na ujenzi wa hiyo barabara kwa kiwango cha lami. Ahsante.