Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 409 2023-05-23

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mlowo – Kamsamba kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza ujenzi wa barabara ya Mlowo – Kamsamba yenye urefu wa kilometa 130.1 kwa awamu kwa kuanza na ujenzi wa Daraja la Momba lenye urefu wa mita 80 pamoja na barabara zake unganishi zenye urefu wa mita 950 na kazi ya ujenzi imekamilika. Aidha, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii. Katika mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imepanga kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Ahsante.