Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Kijiji cha Kalema Maziwani linalounganisha Wilaya za Kiteto, Chemba na Kondoa?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri sana, kwamba tayari kandarasi imeshatangazwa, pamoja na majibu hayo nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, tangu 2019 daraja lilipokatika walitengeneza diversion ambayo magari yote yalikuwa yanapita pale lakini kwa bahati mbaya sasa ile diversion imeharibika kabisa.

Nini mkakati wa Serikali wa kuimarisha hiyo barabara ya mchepuo?

Swali la pili, katika barabara hiyo kutoka Kijiji cha Kalema Maziwani mpaka Mondo, mkandarasi aliyepewa kazi ya kuweka mifereji aliweka chini ya kiwango na hivyo kipindi cha masika maji yale yanaharibu kabisa barabara. Nini kauli ya Serikali juu ya mkandarasi huyu? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu diversion naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa tayari tumeshatangaza tenda na Mkandarasi atakwenda site ni wazi pia kwamba wakati anajenga lazima hiyo diversion aiimarishe. Kwa hiyo, pia nitoe maagizo na maelekezo kwa Meneja wa TANROADS Mkoa wa Dodoma kuhakikisha kwamba anakwenda kuimarisha hiyo diversion ili wananchi na wasafiri wanaopita pale waweze kupita sehemu salama ambapo sasa ni kiangazi, naamini ataitengeneza hiyo diversion.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mifereji. Ni kweli barabara hii tunatengeneza mifereji kwa awamu, tumeendelea kutenga bajeti na hata mwaka huu wa fedha tunakokwenda mifereji itaendelea kutengenezwa. Kwa hiyo, pia nimuagize Meneja wa Mkoa wa Dodoma, kwamba kipindi hiki cha kiangazi ndicho kipindi sahihi cha kutengeneza mifereji, pia niwaombe wananchi wa Chemba kutokufanya shughuli za kijamii karibu na barabara na kuweza kusababisha baadhi ya mifereji kuziba na kuleta changamoto kwenye miundombinu ya barabara. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Kijiji cha Kalema Maziwani linalounganisha Wilaya za Kiteto, Chemba na Kondoa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa hii nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Manyoni Mashariki kuna Daraja la Sanza ambalo upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na ulipaji wa fidia wananchi ulishakamilika. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Daraja la Sanza? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli daraja la Sanza ni kati ya madaraja makubwa ambayo yanaunganisha Mkoa wa Singida na Mkoa wa Dodoma na Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba tulitangaza tenda lakini bahati mbaya sana, Mkandarasi aliyepata hiyo tenda alijitoa na sasa tunaendelea na negotiations na Mkandarasi wa pili kwa maana ya kulijenga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo daraja lilikuwa limepangwa actually liwe limeanza kujengwa katika mwaka huu wa fedha. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba dhamira hiyo ipo, tunaendelea na negotiations na yule mshindi wa pili ili aweze kuanza kulijenga hilo daraja. Ahsante.