Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 408 2023-05-23

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Kijiji cha Kalema Maziwani linalounganisha Wilaya za Kiteto, Chemba na Kondoa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), tayari imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya kujenga upya Daraja la Kalema Maziwani katika barabara ya Kondoa – Bicha – Dalai ambalo lilititia kutokana na mvua kubwa za mwaka 2019. Ili kujenga daraja hilo mnamo tarehe 19 Mei, 2023 Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imetangaza zabuni kwa ajili ya ujenzi na zabuni hizo zimepangwa kufunguliwa Tarehe 05 Juni, 2023, ahsante.