Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, lini Mlima Nkongore utarudishwa kwa Wananchi wa Kata ya Katare baada ya kuchukuliwa na Jeshi la Magereza?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Baada ya wananchi kunyang’anywa ile ardhi, wananchi wa Nkongore mwaka 2020 kabla ya uchaguzi walikuja hapa Dodoma kumwona Waziri Mkuu na Waziri Mkuu aliahidi kwamba, wataenda kurudishiwa lile eneo. Sasa mpaka leo bado hawajarudishiwa na mbaya zaidi hao magereza ambao wamekabidhiwa kwa ajili ya ulinzi kuna shughuli tena wanafanya. Nataka kujua ni kwa nini sasa pale ambapo Serikali imeamua kutwaa ardhi kwa ajili ya matumizi mbadala isiwalipe fidia wananchi? Ni nini taarifa ya fidia ya wananchi wa Nkongore ili waweze kupata kifuta jasho waendelee na shughuli zao ambazo walikuwa wakifanya Serikali inachukua ile ardhi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali pili. Mheshimiwa Waziri ameeleza hapa kwamba, imesababisha kwa sababu ya taratibu za kimazingira wakakabidhi Jeshi la Magereza, ulinzi na usalama, lakini wananchi wale wakati ardhi inachukuliwa walikuwa wamepanda miti ya kudumu pamoja na mazao mbalimbali. Sasa mbaya zaidi askari magereza hawa wanavuna ile miti ya kudumu ya wananchi, wanaenda kufanyia shughuli nyingine. Ni kwa nini sasa kama ile miti inaruhusiwa kuvunwa nje ya hizo taratibu ambazo amezitaja hapa, wasiruhusu wananchi wale wavune miti yao ambayo walikuwa wameipanda kwa ajili ya biashara ili waweze kupata fedha zao stahiki?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili la wananchi kuwalipa fiidia ya maeneo yanayotwaliwa kwa mujibu wa sheria, nimeeleza kwenye jibu la msingi kama Mheshimiwa Mbunge amenisikiliza kwa makini kwamba, maeneo ya milima ni maeneo yanayohifadhiwa. Hakuna mtu anayeweza akadai kwamba, anamiliki mlima, kwa hivyo, kama walikuwa wanafanya shughuli za kibinadamu kando mwa milima ambazo sio sehemu ya mlima tutawasiliana na mamlaka husika, kwa maana ya Mji wa Tarime. Namwomba Mheshimiwa Esther Matiko tukutane baada ya kipindi cha maswali na majibu ili anipe ufafanuzi mzuri, niweze kutoa maelekezo stahiki kwa wenzetu w akule Tarime.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uwepo wa miti iliyokuwa imepandwa na wananchi. Kama kuna uthibitisho huo tutawasiliana na mamlaka husika, kwa maana ya Magereza Mara na Tarime, Rorya, ili waweze kuwaruhusu wananchi wakate miti yao, lakini tunachoshukuru ni kwamba, hata Jeshi la Magereza katika hali ya kutunza ile hifadhi ya mlima wameshaanza kupanda miti na sasa wamepanda karibu miti 1,000 kuzunguka ule mlima kama sehemu ya kuhifadhi mazingira yale, nashukuru.

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, lini Mlima Nkongore utarudishwa kwa Wananchi wa Kata ya Katare baada ya kuchukuliwa na Jeshi la Magereza?

Supplementary Question 2

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kwa kuwa maeneo haya wananchi walikuwa wanalima na wanayatumia kwa ajili ya kujipatia chakula. Je, Serikali haioni haja sasa ya kuwarudishia maeneo haya na ikawasimamia ili waendelee kulima na kuendelea kujipatia chakula?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa swali la Mheshimiwa Ghati, anayetetea wananchi wake wa Tarime, lakini nimweleze kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu langu la msingi ni kwamba, eneo lile limechukuliwa ili kutunza mazingira, lakini pia na kutunza shughuli za usalama ambazo wengine walikuwa wanatumia maeneo yale kulima kilimo cha mazao haramu ya bangi, kwa hiyo, uwepo wa magereza umesaidia kudhibiti hali ile ili isitokee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli, mlima ule uko karibu sana na mjini. Nadhani shughuli za kilimo mijini zinaruhusiwa, lakini huwezi ukasema pale kwa namna mji unavyoendelea kukua patakuwa na maeneo mengi ya kulima zaidi ya kutunza usalama uliopo. Hata hivyo, tutaongea na Mamlaka ya Mji wa Tarime ili kuona kama kweli yako maeneo pembeni ya mlima yanaweza kutumika na wananchi basi wananchi waruhusiwe kuendelea na shughuli zao. (Makofi)