Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 407 2023-05-23

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, lini Mlima Nkongore utarudishwa kwa Wananchi wa Kata ya Katare baada ya kuchukuliwa na Jeshi la Magereza?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge, Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya hifadhi na milima kama ilivyo kwa Mlima Nkongore, kisheria huwa yapo chini ya Halmashauri ya uendelezaji miji husika. Aidha, mwanzoni mwa mwaka 2016 baadhi ya wananchi walianzisha shughuli za kilimo cha mazao mbalimbali ikiwemo mazao haramu ya bangi katika eneo la kuzunguka Mlima Nkongore uliopo chini ya Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia kilimo kilichokuwa kinafanyika katika maeneo ya Mlima Nkongore, pia kutokana na Sheria ya Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004, kifungu cha 58(1) na (2) kinachozuia kufanya shughuli zozote zinazoweza kupelekea hifadhi ya mlima kuharibiwa kwa kuwa maeneo hayo yanatakiwa yahifadhiwe kisheria. Kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya cha tarehe 11 Novemba, 2017 kiliazimia kuwa eneo la Mlima Nkongore likabidhiwe kwa Jeshi la Magereza ili kuimarisha shughuli za ulinzi na usalama. Kupitia barua Kumb. Na. AB.284/311/01C/59 ya tarehe 17 Novemba, 2017 ni idhini rasmi ya kukabidhi eneo la mlima Nkongore kwa Jeshi la Magereza kwa lengo la kuimarisha ulinzi na usalama pamoja na uhifadhi wa mazingira, ahsante.