Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati na kuongeza uwezo wa Gereza la Dimani Wilayani Kibiti?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu yenye kuleta matumaini ya Serikali nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa, Serikali imesema imetenga fedha milioni 350; na kwa kuwa, Gereza la Dimani ni miongoni mwa magereza ambayo yatafanyiwa ukarabati. Je, Serikali inasema nini juu ya nyumba chakavu zilizopo kwenye Gereza hili la Dimani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa, changamoto ya uchakavu wa miundombinu inafanana na Gereza la Kigongoni, Bagamoyo na binafsi niliwahi kulitembelea na nikaona jitihada zao wenyewe askari magereza kwa kujenga nyumba na nikawachangia mifuko 50 ya simenti, lakini bado nyumba nyingine ni chakavu. Je, Serikali ina mpango gani wa muda mrefu wa kuwajengea nyumba askari magereza kwenye magereza mbalimbali kama inavyofanya kwenye majeshi mengine likiwemo Jeshi la JKT na Jeshi la Wananchi? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uchakavu wa nyumba kama pia zitahusika katika ukarabati huu, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, fedha za ukarabati zinapelekwa kwenye gereza. Mkuu wa gereza pamoja na menejimenti yake wataangalia wapi pana tatizo kubwa zaidi na wanalipa kipaumbele katika ukarabati. Hatuta-prescribe, hatutaagiza kwamba, karabati gereza acha nyumba kwa hiyo, kama nyumba zina hali mbaya zaidi wataanza kukarabati nyumba, kama gereza lina hli mbaya zaidi wataanza na gereza. Kwa hiyo, uhuru tunawaachia wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ukarabati wa Gereza la Bagamoyo ambalo pia, Mheshimiwa Mbunge amesema limechakaa sana. Nimhakikishie tu mpango wetu wa ukarabati na ujenzi wa magereza unaenda sambamba kama tulivyokwishasema. Tumeanza mwaka jana, mwaka huu tunaendelea na mwaka ujao pia tutaendelea. Kwa hiyo, gereza la Bagamoyo kulingana na hali ya upatikanaji wa fedha litakuwa moja ya magereza yatakayoingizwa kwenye mpango wa ukarabati. Ahsante sana.

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati na kuongeza uwezo wa Gereza la Dimani Wilayani Kibiti?

Supplementary Question 2

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nilikuwa na swali dogo la kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri. Je, sasa Serikali haioni umefika wakati wa kuboresha magereza haya ambayo yapo Tanzania nzima ambayo Serikali imerithi na kujenga ya kisasa ambayo yataendana na mfumo wa sasa hivi wa teknolojia ambayo hata Mahakama sasa hivi wanaendesha kesi kwa mfumo wa mtandao ambao iepushe Serikali kutumia gharama ya kuwatoa mahabusu hapa na kuwapeleka mahakamani. Je, kwa nini Serikali isijenge magereza mapya ambayo yatakuwa yana mfumo wa kiteknolojia? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba, yapo mabadiliko makubwa ya teknolojia na uendeshaji wa mashauri, hasa Mahakama imeshapiga hatua kubwa. Kwa msingi huo pia, Wizara ya Mambo ya Ndani, kupitia Jeshi la Magereza pia tumeanza. Magereza yanayojengwa sasa yanazingatia mahitaji hayo ya teknolojia na mengine yaliyo bora zaidi ikiwemo pamoja na ukaguzi, vitawekwa vifaa vya elektroniki, ili kuepusha watu kuguswaguswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa magereza ambayo tunayo haiwezekani yote tuyabadilishe siku moja. Tutaendelea kuyakarabati, yatakayofaa kuingiziwa vitendea kazi vya kisasa, vifaa vya kisasa zaidi, tutafanya hivyo, lakini mengine tutaendelea kuyakarabati ili yatoshe kulingana na uwezekano wa bajeti tutaimarisha kwenda kama anavyoshauri Mheshimiwa Mbunge katika siku zijazo, ahsante.