Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 406 2023-05-23

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE K.n.y. MHE. SUBIRA K. MGALU aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukarabati na kuongeza uwezo wa Gereza la Dimani Wilayani Kibiti?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Twaha Ally Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali itatenga fedha shilingi milioni 350 kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa baadhi ya Magereza nchini. Gereza la Dimani Wilaya ya Kibiti ni moja ya magereza yatakayokarabatiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali, kupitia mpango na bajeti wa kila mwaka itaendelea kutenga fedha za ukarabati na upanuzi wa Magereza yenye uhitaji huo, ahsante.