Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: - Je, upi mkakati wa kutokomeza wizi wa dawa na vifa vya afya, hatua zilizochukuliwa kwa wahusika na fedha zinazopotea kwa mwaka?

Supplementary Question 1

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu hayo mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, kwa kuwa tathimini iliyofanywa na Wizara Novemba 2021 ilibaini kwamba jumla ya bilioni 83 za bidhaa za dawa pamoja na bidhaa za afya zilikuwa zimeibiwa.

Je, Serikali ilichukua hatua gani na imechukua hatua gani kwa hao watumishi ambao wamefanya ubadhilifu wa dawa hizo kwa ajili ya wananchi kwa ajili ya kutolea huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa, uwezo wa Bohari ya Dawa (MSD) kusambaza dawa pamoja na bidhaa nyingine za afya ni asilimia 59 tu. Hii inatokana na malimbikizo ya madeni ambayo ni zaidi ya bilioni 259, lakini pia mtaji wa bilioni 593. Je, Serikali inatoa tamko gani kumaliza matatizo haya, ili kuiwezesha taasisi yetu ya MSD kuwa na uwezo mkubwa wa kusambaza dawa pamoja na bidhaa nyingine za afya kwa maslahi ya wananchi wetu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimshukuru Mbunge mwenzangu kwa swali lake zuri, lakini swali la kwanza ni kwamba, wamechukuliwa hatua gani wale walioonekana kufanya ubadhiriru wa bilioni 83. Moja, sisi kama wataalam wa Wizara ya Afya tulifanya kazi yetu na kuona kwamba, kuna dalili za upotevu wa bilioni 83.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi yetu iliyofuata ni kukabidhi kwenye taasisi yetu ya TAKUKURU ambayo ina wataalam wa kujua sasa ili kufuata sheria na taratibu na haki za watumishi wa umma, tumepeleka kule wanafanya uchunguzi. Miezi miwili iliyopita walituambia kwamba, wako kwenye hatua za mwisho sasa kuweza kubaini specifically ni nani kafanya nini na ni nini kimefanyika ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua. Hilo ni swali lake la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, ni kweli kwamba, Waheshimiwa Wabunge fedha wanazopitisha hapa bilioni 200 kwa ajili ya vifaa tiba na dawa ni fedha za vituo vyetu kwenye majimbo yetu. Maana yake tukipitisha hapa kwenye bajeti tunapitisha pesa kwa ajili ya vituo vyetu. Vituo vyetu vikipata pesa zinapelekwa MSD, maana yake ni nini? MSD tulitegemea i- operate kama bohari ya dawa, lakini ina-operate kama procurement entity.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hilo la kwamba, wapewe mtaji, nafikiri liliibuka wakati wa bajeti yetu na Wizara ya Fedha wamelichukua na wiki iliyopita tulikutana kujadili kuona namna gani MSD wanaweza wakapatiwa mtaji, ili sasa tukiwapitishia fedha hapa Bungeni, basi vituo vyetu vikiomba dawa MSD wakutwe tayari walishanunua dawa hizo. Hilo ni suala la kulichukua tu ili kuondoa ucheleweshaji uliopo.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: - Je, upi mkakati wa kutokomeza wizi wa dawa na vifa vya afya, hatua zilizochukuliwa kwa wahusika na fedha zinazopotea kwa mwaka?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya mwaka jana tulipata bahati ya kupita naye katika baadhi ya zahanati zetu Wilayani Serengeti alishuhudia upungufu mkubwa wa dawa na vifaa tiba. Sasa je, ni lini na kuna mpango gani wa kuhakikisha uwepo wa dawa na vifaa tiba vya kutosha katika zahanati ya Kemgesi, Maburi, Busawe, Nyansulula, Mbalibari, Koleli, Rubanda, Kituo cha Afya Nata na Zahanati ya Rigita? Ahsante.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulikuwa naye pamoja Serengeti, tuliona hilo tatizo. Sasa namwagiza DMO wa Serengeti leo aandike mahitaji ya hiyo hospitali na wiki hii watapata dawa.