Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 404 2023-05-23

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza: -

Je, upi mkakati wa kutokomeza wizi wa dawa na vifa vya afya, hatua zilizochukuliwa kwa wahusika na fedha zinazopotea kwa mwaka?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina, Mbunge wa Kisesa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Suala la kupambana na wizi na ubadhirifu wa bidhaa za afya si la Serikali pekee bali ni suala letu sisi wote, hasa wawakilishi wa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali katika kutatua tatizo la wizi wa dawa na vifaa tiba kama ifuatavyo: -

a) Kufanya agenda ya ulinzi wa bidhaa za afya kuwa agenda ya kudumu katika vikao vya kamati za ulinzi na usalama za mikoa na wilaya.

b) Kujenga uwazi wakati wa kupeleka bidhaa za afya na kuwapa wakuu wa wilaya na Wabunge nyaraka za makabidhiano ya dawa na vifaa tiba kwa ajili ya rejea.

c) Kuimarisha mifumo ya usimamizi wa bidhaa za afya ikiwemo kufunga mifumo ya kielektroniki pamoja na kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara.

d) Kuimarisha kamati za usimamizi za vituo kwa kuzijengea uwezo kuhusu majukumu yao katika usimamizi wa bidhaa za dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ilifanya uchunguzi wa ubadhilifu wa bidhaa za afya na taarifa kuwasilishwa kwenye semina ya wabunge, na kupelekwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili kufanya thamani halisi ya bidhaa zilizopotea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.