Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isikae na taasisi za afya za kidini Wilayani Muleba ili kupunguza changamoto zilizopo katika kutoa huduma?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa taratibu kama hizo kama alivyoeleza Mheshimiwa Naibu Waziri zipo, lakini utekelezaji wake wakati mwingine unaleta changamoto;

Je, ni kwa nini Serikali sasa isifuatilie kujua hatma ya yale mazungumzo yanakuwaje ili mwisho wa siku wananchi wapate huduma wanazozitarajia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili. Kituo cha Afya cha Nakatunguru Jimboni Ukerewe ni muhimu sana, kinahudumia watu zaidi ya 10,000 kwenye Mji wa Nansio pale lakini kina upungufu mkubwa wa miundombinu;

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa miundombinu kwenye kituo kile cha afya cha Nakatunguru ili kiweze kutoa huduma zinazostahili kwa wananchi wa ukerewe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi katika majibu yangu ya msingi kwamba utaratibu upo wa kamati hizi za kitaalamu za kushauri katika ngazi ya mkoa. Kuna timu ya mkoa, kuna timu ya halmashauri na mashirika ya kidini ambayo yanamiliki hospitali hizi. Kwa hiyo nipende kuchukua nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kuwataka waganga wote wakuu wa mikoa hapa Tanzania kuhakikisha wanakaa vikao hivi ambavyo vipo kisheria na wenzetu wamiliki wa hospitali hizi ambao ni taasisi za kidini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kweenye swali lake la pili la kituo cha Nakatunguru kule Nansio Ukerewe, kwamba ni lini Serikali itapeleka fedha kumalizia. Serikali itapeleka fedha kumalizia kituo hiki kadri ya upatikanaji wa fedha.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isikae na taasisi za afya za kidini Wilayani Muleba ili kupunguza changamoto zilizopo katika kutoa huduma?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi. Kwa kuwa changamoto za hospitali za kidini inaikumba pia hospitali ya Mbagala Mission kwa jina jingine kwa Buluda, ni hospitali ya muda mrefu, na wananchi wote wa Mbagala na maeneo mengine ya Dar es Salaam wanaitegemea sana hospitali hiyo;

Je, Serikali haioni haja kuwaongezea nguvu kituo kile cha Consolata Sisters Mbagala Mission ili waweze kusaidia vizuri zaidi wananchi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nirejee tena majibu yangu ya msingi, kwamba Serikali inao utaratibu wa kukaa na hospitali hizi teule katika maeneo mbalimbali hapa nchini na kama nilivyokwisha toa maelekezo kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI kwa waganga wakuu wote wa mikoa kuhakikisha wanakaa kuangalia uendeshaji wa hospitali hizi teule na kuona ni namna gani ambavyo zinaweza zikaboreshewa huduma zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongezee tu kwa faida ya Bunge lako Tukufu, kwamba Serikali hupeleka watumishi katika hospitali hizi teule lakini vile vile inapeleka mgao wa fedha katika hospitali hizi teule kuweza kusaidia ili wananchi wa maeneo hayo waweze kupata huduma ambayo wanastahili.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE aliuliza: - Je, kwa nini Serikali isikae na taasisi za afya za kidini Wilayani Muleba ili kupunguza changamoto zilizopo katika kutoa huduma?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia watu wengi sana kwa sababu jiko barabarani pale, watu wa kutoka Mufindi wanahudumiwa pale lakini miundombinu yake ni chakavu;

Je, ni lini Serikali itakarabati miundombinu hiyo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itakarabati miundombinu hii chakavu pale katika Hospitali ya Mji Mafinga kadri ya upatikanaji wa fedha. Lakini nirudie tena kwamba Wakurugenzi wa Halmashauri wana wajibu wa kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kuanza kutengeneza miundombinu mbalimbali kwenye halmashauri zao. Tayari Serikali kuu mmeona imefanya mengi chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka fedha nyingi kwenye halmashauri hizi. Ni wakati umefika kwa wakurugenzi, mabaraza ya madiwani nao kuweka kipaumbele cha kusaidia wananchi pale na kuujnga mkono juhudi ambazo Serikali hii ya awamu ya sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya kwa kupeleka fedha nyingi kwenye sekta hizi za elimu na afya.