Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 403 2023-05-23

Name

Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI K.n.y. MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE aliuliza: -

Je, kwa nini Serikali isikae na taasisi za afya za kidini Wilayani Muleba ili kupunguza changamoto zilizopo katika kutoa huduma?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles John Mwijage, Mbunge wa Jimbo la Muleba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Muleba ina vituo sita vya kutolea huduma za afya vinavyomilikiwa na mashirika ya kidini. Hospitali tatu za Lubya, Ndolage na Kagondo, Kituo cha Afya kimoja na zahanati mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inao utaratibu wa kukaa na hospitali teule za wilaya kupitia bodi ambazo zimejumuisha wataalam wa kutoka ngazi ya mkoa na halmashauri husika. Bodi hizo hukutana kila robo mwaka kwa ajili ya kupitia taarifa za utendaji pamoja na kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza wakati wakutoa huduma.