Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Kituo cha Afya cha Msanda Muungano katika Tarafa ya Mpui?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa ya maswali madogo ya nyongeza. Nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa maneno yenye matumaini kwa wananchi wa Kata ya Msanda Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza. Serikali imetumia fedha takribani shilingi 500,000,000 kujenga kituo cha afya katika Kata ya Kipeta, Tarafa ya Kipeta lakini mpaka sasa haijapeleka vifaa tiba;

Je, ni lini Serikali itapeleka vifaa tiba kwenye kituo hiki ambacho kilisubiriwa kwa muda mrefu na wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Serikali ilipeleka fedha takribani shilingi milioni 100 kwa ajili ya kujenga zahanati katika Vijiji vya Nderema, Mpembano, Mpona na Lyapona, lakini mpaka sasa zahanati hizo zimekamilika na hazina vifaa tiba;

Je, ni lini sasa Serikali mtapeleka vifaa tiba?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumpongeza Mheshimiwa Sangu, kwa sababu ni majuzi tu alikuja ofisini kwa ajili ya kuangalia zahanati hizi katika Jimbo lake la Kwela. Tayari kuna milioni 150 ambayo imetengwa. Kwenye swali lake la kwanza imetengwa shilingi milioni 150 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba kwenye bajeti hii ya 2022/2023.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile nikienda kwenye swali lake la pili; kwenye zahanati zilizokamilka vilevile imetengwa shilingi milioni 50 kwa jili ya ununuzi wa vifaa tiba. Na fedha hizi mtakaponunua vifaa tiba pale Sumbawanga DC ninyi ndio mtaamua viende kwenye vituo vipi; lakini priority iwe katika hivi ambavyo vimekamilika na vinasubiri kutoa huduma kwa wananchi.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Kituo cha Afya cha Msanda Muungano katika Tarafa ya Mpui?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tarafa ya Nkwenda ina kituo cha afya kimoja na kituo hiki kimezidiwa na wagonjwa wengi;

Je, ni lini Serikali itajenga kituo ha afya kwenye kata ya Songambele ambako tayari tulishaleta maombi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la Mheshimiwa Bilakwate linalohusiana na Tarafa ya Nkwenda kuzidiwa; ni adhma ya Serikali kuhakikisha inajenga vituo vya afya katika kata za kimkakati kote nchini ikiwemo Jimbo lake lile la Kyerwa. Tutaangalia katika bajeti ya 2023/2024 kama imetengwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya. Kama haikutengwa tutatenga fedha katika mwaka wa fedha 2024/2025 kadri ambavyo fedha itapatikana.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Kituo cha Afya cha Msanda Muungano katika Tarafa ya Mpui?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wananchi wa kata ya Kenyamanyoli waliamua kujenga kituo cha afya kwa nguvu zao wenyewe, kwa maana Kituo cha Afya cha Kenyamanyoli, lakini Serikali iliahidi kupeleka fedha kuanzia mwaka 2019 kwa ajili ya umaliziaji wa maboma yale, mpaka leo hawajapeleka. Ningetaka kujua ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa yale maboma ili wananchi wa Kenyamanyole waweze kupata huduma ya afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kipaumbele cha Serikali kuhakikisha inaunga mkono jitihada za wananchi popote pale nchini ambapo wamejitoa kujenga huduma mbalimbali wao wenyewe kwenye jamii yao; na Serikali itatafuta fedha kadri ya upatikanaji wake ili iweze Kwenda kuunga mkono hujudi hizo katika Kituo hiki cha Afya cha Kenyamanyoli. Vilevile nichukue nafasi hii kumuelekeza Mkuruhenzi wa kule Tarime Mjini, kuhakikisha anatenga fedha kwenye mapato yake ya ndani kuunga mkono jitihada hizi za wananchi wa Kenyamanyoli.