Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, lini barabara ya Mombo Mzeri itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na majibu ya Serikali nina mswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, barabara hii ni mihimu sana, ndiyo barabara fupi na rahisi kuunganisha Kijiji cha Msomela Kijiji cha mfano, na barabara kubwa ya Segera - Arusha. Sasa kwa sababu ya umuhimu huo;

Je, ni lini Serikali itakubali kuipandisha hadhi barabara hii iwe barabara ya Mkoa ihudumiwe na TANROADS, barabara hii pamoja na zile barabara nyingine kama ile ya Msambiazi - Lewa - Lutindi na barabara ya Kwetonge – Tonge – Kizara?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Mvua zinazonyesha sasa hivi Korogwe zimeathiri sana barabara zetu za changarawe;

Je, Serikali iko tayari kuwapa TARURA fedha za dharura ili wakatusaidie kurekebisha hali ya barabara zetu kwenye maeneo ambayo yameathiriwa na mvua?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikubaliane na Mheshimiwa Mnzava kwamba barabara hii ni muhimu sana na barabara hii pia imetajwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2025 Ibara ya 55(c)(4) katika ukurasa wa 77. Hivyo ni kipaumbele cha Serikali kuhakikuisha barabara hii inajengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kupandisha hadhi taratibu ziko wazi za kisheria, inatakiwa wao kule waaanze katika vikao vyao vile vya DCC itoke pale ipite katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa, na ikitoka kwenye Bodi ya Barabara ya Mkoa waende wapitishe kwenye RCC na iwasilishwe kwa Waiziri mwenye dhamana na TANROADS ambaye ni Waziri wa Ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili; fedha za dharura kwa TARURA, tayari Serikali inaliangalia hilo na tayri ilikuwa bajeti yao TARURA wao kwa mwaka ya dharura ilikuwa ni bilioni 11. Hivi sasa tunaangalia namna ya kuweza kuwaongezea fedha Kwenda mpaka bilioni 43 ili kuhakikisha kwamba wana fedha ya kutosha ya dharura kwa ajili ya ujenzi wa barabara wakati wote; ije mvua lije jua barabara ziwe zinapitika na ndiyo maana Serikali pia imeiongezea TARURA bajeti kubwa sana kutoka bilini 226 mpaka bilioni 776.

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, lini barabara ya Mombo Mzeri itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Barabara hii iliyotajwa na Mheshimiwa Mnzava lini Serikali wataanza kuiwekea changarawe ili angalau ianze kupitika wakati wote maana kwa sasa kuna maeneo mengi hayapitiki.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi ni barabara ambayo ipo kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, na inaunganisha pia wilaya mbili. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 barabara hii ilitengewa shilingi milioni 230 kwa ajili ya ukarabati wa kiwango cha changarawe, na Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa barabara hii kuhakikisha makalavati yanapitika lakini pia na ule upembuzi yakunifu kwa ajili ya kuwa barabara ya lami.