Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 31 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 401 2023-05-23

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, lini barabara ya Mombo Mzeri itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Mombo - Mzeri ina urefu wa jumla ya kilometa 30 inayounganisha barabara kuu ya Segera – Same na Makao Makuu ya Kata ya Magambakwalukonge, Mkalamo na Wilaya ya Handeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaanza kufanya Upembuzi yakinifu na Usanifu wa kina katika barabara hii na kazi hii inatarajiwa kuanza katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 ili kupata gharama halisi za ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA imeendelea kuimarisha barabara hii kwa kiwango cha changarawe pamoja na kujenga vivuko na makalavati ili kuhakikisha inapitika majira yote ya mwaka.