Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 1

MHE. BENAYA L KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri ambayo yanatia moyo wananchi hawa wa Wilaya ya Mbinga kwa maana ya barabara hii ya Litembo ambayo imesubiriwa kwa muda mrefu na inaahadi za Marais Watatu kujengwa kwa kiwango cha lami, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Matiri kwa maana ya Kigonsera hadi Matiri ambako kuna kilimo kikubwa cha maharage na mahindi inapitika kwa shida sana, sasa wakati tunasubiri mchakato huo kuendelea, Serikali inampango gani wa kuifanya hii barabara iweze kupitika kwa msimu mzima?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, barabara ya kutoka Liyombo kuja hadi Rwanda kupitia Mdunduwalo ambayo Makaa ya Mawe yanapita hivi sasa ama haipitiki baadhi ya siku, ama inapitika kwa shida sana, tumeleta maombi maalum ni lini sasa Serikali itaitengeneza barabara hii kupitisha makaa ya mawe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Matiri - Kigonsera kama alivyoisema kweli ni barabara ya changarawe ambapo sasa hivi ni kipindi kikubwa ambacho mvua kubwa sana inanyeesha naomba nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeshatoa taarifa kwa mameneja wote wa TANROADS Tanzania kuhakikisha kwamba barabara zote ambazo zinachangamoto waweze kuzisimamia kwa ukaribu na narudia tena kumsisitiza Meneja wa Mkoa wa Ruvuma ahakikishe kwamba barabara ya Matiri – Kigonsera inapitika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala lake la pili la kutoka Liyombo hadi Rwanda hii ndiyo barabara ambayo inasafirisha sana Makaa ya Mawe na kuna migodi kama minne, ambayo pia Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo tuweze kuitengeneza.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii tutahakikisha kwamba inapitika na kama nilivyosema kwamba kwenye barabara zingine Mkandarasi yuko site kwenye hayo maeneo lakini inategemia na hali ya hewa. Kwa hiyo, Mkandarasi yuko site kuhakikisha kwamba patakapotokea nafuu ya hali ya hewa wataendelea kuitengeneza hiyo barabara ili iweze kupitika. Ahsante. (Makofi)

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba kufahamu ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya kutujengea barabara ya Mlowo – Kamsamba? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, babrabara ya Mlowo - Kamsamba naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira ni barabara ambayo imepigiwa sana kelele katika Bunge hili, kwa hiyo tunategemea kwamba itakuwa kwenye mapendekezo kwa ajili ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 3

MHE. NORAH W. MZERU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati barabara ya Isimilo - Kilombero ili kuwasaidia wakulima kupitisha mazao yao kwa urahisi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii naamini inatengenezwa na inakarabatiwa, changamoto kubwa ambayo tunayo sasa hivi ni barabara nyingi katika kipindi hiki cha mvua kunatokea changamoto, pia nitoe tu maelekezo tena kwa Meneja wa Singida kuhakikisha kwamba anaisimamia hii barabara na inapitika muda wote wakati huu wa kilimo kwa wananchi, ahsante.

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya Makambako - Songea hasa eneo la Madaba kuanzia Igewisinga mpaka Mtiangimbole limebomoka vibaya sana kiasi cha kuhatarisha usalama wa watumiaji. Je, ni lini sasa Serikali itaijenga hii barabara kwa uhakika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nimemuelewa vizuri hii ni barabara kubwa ya kutoka Makambako kwenda Songea, hii barabara ipo kwenye mpango wa kukarabatiwa na World Bank, sasa hivi tutaanzia Lutukila kwenda Songea ikiwa ni pamoja na bypass ya Songea Mjini, wakati huo sasa inatafutwa fedha kuanzia Makambako hadi Lutukila.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 5

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Kwa kuwa, Serikali imeshatoa Milioni 300 kwa ajili ya upembuzi wa barabara ya kutoka Kahama - Nyang’wale – Busolwa - Busisi - Sengerema kwa kiwango cha lami, na huwa unanijibu majibu ya kisiasa nataka leo unijbu, ni lini upembuzi huo utakamilika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tukishatenga fedha kwenye bajeti nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Awamu ya Sita iko makini, ikishatenga maana yake tunatekeleza, isipokuwa tu ni hatua kuwa hatua ndefu.

Mheshimiwa Spika, barabara inayotwa siyo barabara fupi Kahama Nyang’wale - Ngoma hadi Busisi ni parefu, kwa hiyo iko tayari inafanyiwa kazi nakuhakikishia baada ya kukamilika ndiyo sasa tutajua gharama ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 6

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, ahsante; je, ni lini barabara ya Bariadi – Ngulyati kwenda Magu itajengwa kwa kiwango cha lami kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sabu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pia hii barabara ni kati ya barabara ambazo zimeongelewa sana. Namwomba Mheshimiwa Mbunge tusubiri, tutakapoleta bajeti yetu watupitishie, na ninaamini itakuwa ni moja ya barabara ambazo zitakuwepo kwenye mpango, ahsante.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 7

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Barabara ya Iringa – MR – Itunundu iko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi zaidi ya miaka 30. Ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge, kwanza itatakiwa iingizwe kwenye usanifu wa kina, baada ya hapo tukishafanya hiyo kazi, ndiyo tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, tunatambua kwamba iko kwenye Ilani, ifanyiwe usanifu na ninaamini kazi hiyo tutaifanya katika kipindi hiki cha miaka mitano, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 8

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Barabara ya kutoka Hoteli Tatu – Pande – Lihimalyao iko chini ya TARURA, lakini Bodi ya Barabara pamoja na Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Lindi ilipendekeza barabara hii iapandishwe hadhi, ichukuliwe na TANROADS; ni lini TANROADS itaichukua barabara hii? (Kicheko)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge aweze kuleta swali mahususi, ahsante. (Makofi)

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 9

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kilometa 52 kutoka Kilindoni mpaka Rasi Mkumbi, Kisiwani Mafia ni lini zitakamilika kwa ujenzi wa lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyotaja Mheshimiwa Mbunge tumeitengea bajeti mwaka huu unaoendelea na tutaendelea kuitengea katika mwaka unaokuja hiyo barabara ambayo iko katika Kisiwa cha Mafia, ahsante. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Supplementary Question 10

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Tumeshuhudia mvua kubwa zinazoendelea nchi nzima na kufanya mawasiliano katika baadhi ya maeneo kukatika na hivyo kuchukua muda mrefu kuzitengeneza kwa wakati ili wananchi waweze kuendelea na usafiri na usafirishaji, lakini kuokoa uhai wa watu kwa wale ambao labda wanahitaji huduma hizo kwenda hospitali na vinginevyo: -

Nini mkakati wa Serikali wa haraka endapo inatokea changamoto ya namna hiyo, inafanyika kwa haraka na mawasiliano yanarudi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cecilia Paresso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunategemea tutaoa taarifa, kama alivyoongea hata juzi Mheshimiwa Kunambi. Barabara nyingi ambazo tunazo Tanzania, ni Kilometa kama 36,000 ambazo tunazihudumia. Kati ya hizo, ni kilometa 12,000 tu ambazo zina lami. Kwa hiyo, barabara hizi zenye urefu wa kilometa kama 24, nyingi ni za changarawe na nyingine zipo mabondeni ambazo tumeshatoa taarifa kwa wakuu wa barabara kwa maana ya Meneja wa TANROADS kuhakikisha kwamba barabara zote ambazo zinakuwa na changamoto wanazi-attend kwa muda.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ambapo ni kwenye madaraja, tuna madaraja ya muda ya chuma ambayo kama ni daraja linaweza lakini bahati mbaya unakuta siyo tu daraja limeondoka, lakini ni tuta pengine la kilometa moja mpaka mbili limeondoka na wakati mvua inanyesha inakuwa ni ngumu kuweza kufanya hiyo kazi wakati pana maji, ahsante.