Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 184 2023-04-27

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. BENAYA L. KAPINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami barabra ya Kigonsera hadi Matiri na Mbinga hadi Litembo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Liuka Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imetangaza zabuni kwa ajili ya kupata Mhandisi Mshauri wa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara ya Mbinga – Litembo – Mkiri sehemu ya Mbinga – Litembo/Mbuji kilometa 22 kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami ambapo zabuni zimefunguliwa tarehe 19 Aprili, 2023 na uchambuzi wa zabuni unaendelea. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana Serikali itatafuta fedha za kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Spika, aidha, kwa barabara ya Kigonsera – Matiri – Mbaha kilometa 55, Serikali inaendelea kutafuta fedha za kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.