Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa Ndege Lindi kwa kiwango cha lami pamoja na kukarabati Uwanja wa Ndege Nachingwea?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante. Viwanja hivi vilitumika kwa kupigania uhuru Kusini mwa Bara la Afrika. Je, ni nini tamko la Serikali hasa kwamba viwanja hivi lini vitawekwa lami vyote viwili?

Swali pili, Je, ni lini wananchi waliotwaliwa maeneo yao kwa ajili ya kuongeza eneo kwenye uwanja wa ndege wa Nachingwea watalipwa fidia zao? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni lini vitajengwa viwanja hivi, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wote wa maeneo hayo kwamba katika bajeti ya mwaka huu Kiwanja cha Lindi kimetengewa ama tumetenga takribani bilioni 2.5 na fedha hizi zitatumika kwa ajili ya Mkandarasi Mshauri ambae ataandaa document kwa Ajili ya kutangaza viwanja hivi ili viweze kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, suala la pili anataka kuja ni lini wananchi watalipwa fidia. Ni kweli tathmini imekwishafanyika na mwezi Machi daftari ambalo limeshaandaliwa kwa ajili ya malipo liliwasilishwa kwa Mthamini Mkuu na Mthamini Mkuu ataleta Wizarani na Wizara tutapeleka Wizara ya Fedha kwa ajili ya kulipa fidia wananchi hawa katika kiwanja hiki cha Nachingwea. Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa Ndege Lindi kwa kiwango cha lami pamoja na kukarabati Uwanja wa Ndege Nachingwea?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kutokana na umuhimu wa Serikali kukuza utalii hususani katika mbuga yetu ya Burigi – Biharamulo, naomba kujua ni lini sasa uwanja wa ndege wa Biharamulo sasa utakarabatiwa ili uweze kuwa kiungo muhimu cha kuleta watalii katika eneo letu? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Spika, Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Chiwelesa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Kiwanja cha Ndege cha Biharamulo ni miongoni mwa viwanja 11 ambavyo tumevitengea fedha na kwa kiwanja cha Biharamulo pekee tumetenga takribani Milioni 400 kwa jili ya ukarabati kiwanja hiki cha Biharamulo. Ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa Ndege Lindi kwa kiwango cha lami pamoja na kukarabati Uwanja wa Ndege Nachingwea?

Supplementary Question 3

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.

Je, ni lini uwanja wa ndege wa Bukoba Mjini utawekewa taa na mnara wa kuongoza ndege ili kuongeza usalama wa watumiaji wa uwanja huo? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Spika, ahsante. Kiwanja cha ndege cha Bukoba kwenye mwaka wa fedha ujao na kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais tumetenga takribani bilioni 2.9 kwa ajili ya ujenzi wa control tower pamoja na taa za kuongozea ndege katika kiwanja hiki, ahsante.

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa Ndege Lindi kwa kiwango cha lami pamoja na kukarabati Uwanja wa Ndege Nachingwea?

Supplementary Question 4

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri, Wilaya ya Mbogwe ni kubwa iliyo na vyanzo vingi vya mapato, tumeshatenga eneo la kujengewa uwanja wa ndege tayari. Lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Mbogwe? (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge naomba mara baada ya kipindi cha maswali na majibu nionane naye ili niweze kuangalia bajeti kiasi gani tumetenga kwa bajeti ijayo katika eneo lake. Ahsante.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa Ndege Lindi kwa kiwango cha lami pamoja na kukarabati Uwanja wa Ndege Nachingwea?

Supplementary Question 5

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Lake Manyara Airport utajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE):
Mheshimiwa Spika, uwanja alioutamka Mheshimiwa Mbunge ni miongoni mwa viwanja ambavyo vipo chini ya Benki ya Dunia na tayari tupo katika mchakato wa kutangaza tenda ili viwanja hivi viweze kujengwa kikiwemo na Kiwanja cha Tanga, ahsante. (Makofi)