Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 183 2023-04-27

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga uwanja wa Ndege Lindi kwa kiwango cha lami pamoja na kukarabati Uwanja wa Ndege Nachingwea?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ,napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha kazi ya kufanya marejeo ya usanifu wa kina kwa ajili ya ukarabati na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Lindi kwa kiwango cha lami. Marejeo ya usanifu wa kina yalifanyika ili kuzingatia mahitaji ya sasa ya kiwanja, ikiwemo kuwezesha utekelezaji wa Mradi wa Gesi katika maeneo hayo. Kwa sasa, Serikali inakamilisha maandalizi ya makabrasha ya zabuni hiyo ili iweze kutangazwa.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kiwanja cha Ndege cha Nachingwea, Serikali imekuwa ikifanya matengenezo ya miundombinu ya kiwanja hicho ili kiendelee kutumika ambapo mwaka 2020 ilikamilisha ukarabati mkubwa wa barabara ya kuruka na kutua ndege kwa kiwango cha changarawe.

Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa Kiwanja cha Ndege Nachingwea, Serikali inaendelea na utwaaji wa eneo la ziada ili kujenga kiwanja hicho kwa kiwango cha lami. Aidha, mnamo mwezi Machi, 2023 wataalam wa Wizara walifanya uhakiki wa daftari la fidia na kuwasilishwa kwa Mthamini Mkuu wa Serikali kwa idhini, ahsante.