Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kivuko kipya ya Kigamboni utaanza baada ya kutengewa fedha mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, naomba nimuulize Naibu Waziri maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa mwaka wa fedha 2023/2024 umebaki miezi miwili.

Je, ni lini wananchi wa Kigamboni watarajie vivuko hivyo viwili vidogo kama Mheshimiwa Naibu Waziri anavyoongea?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa TEMESA ni Taasisi ya Umma inayotoa huduma za ufundi na umeme pamoja na huduma za vivuko.

Je, Serikali haioni sasa umefika muda muafaka wa kushirikisha sekta binafsi katika kutoa huduma ya vivuko ili kuongeza ufanisi na kuongeza wigo wa huduma hususani kwa wananchi wa Kigamboni?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, mwaka huu tulitegemea tuanze manunuzi ama utengenezaji wa kivuko na kazi hiyo tumeshaanza, kwa sababu tulitangaza tenda kununua hivi vivuko viwili lakini ilionekana watu hawa walikuwa wame-bid, wote walikuwa wame-tender bei za juu wakati wa kufanya evaluation, hivyo tunatangaza upya tena tenda, kwa hivyo tupo kwenye utekelezaji wa bajeti ya mwaka huu.

Mheshimiwa Spika, niwahakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kigamboni na Magogoni kwamba hizo taratibu zinaendelea tutakapopata Mkandarasi sahihi shughuli hizo zitaanza mwaka huu wa fedha na tayari tumeshaanza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, tayari yalikuwa pia ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba taasisi zote ambazo zinafanya biashara kama kuna uwezekano wa watu binafsi kufanya biashara basi waruhusiwe, hivi ninavyoongea tayari Azam ameshaonesha nia ya kutaka kufanya shughuli katika kivuko hiki cha Kigamboni na sasa itakuwa ni kwa vivuko vyote tunategemea Serikali ikishakamilisha taratibu basi wale wafanyabiashara ambao wanataka kufanya biashara sambamba na TEMESA taratibu zikishakamilika wataruhusiwa kufanya hivyo. Ahsante.(Makofi)

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kivuko kipya ya Kigamboni utaanza baada ya kutengewa fedha mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 2

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ninataka nijue tu ni lini Serikali itarejesha kituo cha MV Musoma kilichokuwa kinatoa huduma kati ya Kinesi kwa maana ya Rorya na Musoma Mjini hasa ukizingatia kituo kilichopo ni kidogo na hakikidhi mahitaji ya watu lakini pia ni hatari kwa maisha ya wananchi wake? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kivuko cha Musoma - Kinesi kiliazimwa kwenda kufanya kazi kati ya Kisolya na Lujezi, Musoma tulipeleka kivuko cha Chato One. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunategemea mwishoni mwa mwezi huu Tarehe 30 Kivuko cha Kisolya- Lugeza ambacho kilikuwa kinatengenezwa kitakamilika na mwanzoni mwa mwezi unaokuja kivuko cha MV Musoma kitarudishwa kwa ajili ya kutoa huduma iliyokuwa imezoeleka kati ya Musoma na Kinesi. Ahsante.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kivuko kipya ya Kigamboni utaanza baada ya kutengewa fedha mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 3

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, kwenye mradi wa SGR kwenye eneo la Kikongo pamoja na Msuwa kuna uhitaji wa kuweka kivuko na TRC waliahidi kuweka ni muda mrefu sasa.

Je, Waziri atakuwa yuko tayari kutoa agizo kwa Mkururgenzi wa TRC kukamilisha mradi huo kabla haujaanza utekelezaji wake?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwakamo Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumejadili na Mheshimiwa Mbunge na tayari nilishatoa maelekezo kwa Mtendaji wa TRC ili waweze kuangalia eneo hilo ambalo ni muhimu sana kuwa na kivuko kwa waenda kwa miguu ili waweze kuangalia uwezekano wa kujenga kivuko mahali aliposema Mheshimiwa Mbunge, ahsante.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kivuko kipya ya Kigamboni utaanza baada ya kutengewa fedha mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 4

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Gati la kushukia abiria jengo la mizigo ya wasafiri, jengo la abiria Bandari ya Manda Wilayani Ludewa utaanza lini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Gati la Manda upo kwenye mpango, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutahakikisha kwamba tunajenga gati hili la Manda ili wananchi wasipate changamoto ambayo wanaipata sasa hivi, ahsante.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kivuko kipya ya Kigamboni utaanza baada ya kutengewa fedha mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 5

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, Serikali imetoa pesa nyingi sana kwa ajili ya ujenzi wa kivuko cha Mwaya – Kajunjumele; je, ni sababu gani zinafanya mpaka sasa hivi kisianze kufanya kazi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kati ya Mwaya- Kajunjumele tuna kivuko ambacho kilitoka Luhuhu kiko site na tunachosubiri sasa hivi ni kwamba maji yaweze kupungua ili tuweze kurekebisha rampu halafu baada ya hapo kivuko hicho kitaanza kutoa huduma kati ya Mwaya na Kajunjumele, ahsante.

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa kivuko kipya ya Kigamboni utaanza baada ya kutengewa fedha mwaka 2022/2023?

Supplementary Question 6

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Katika Jimbo la Singida Kaskazini Kijiji cha Kinyeto na Ilongero kuna bwawa la Ntambuko ambalo wananchi wanapata shida...

SPIKA: Swali lako.

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, ni lini sasa Serikali italeta kivuko katika bwawa la Ntambuko linalounganisha Kijiji cha Itamuka, Ilongero na Kinyeto?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba tumelichukua hilo na TEMESA watakwenda kufanya study ili waone kama kivuko kinaweza kikajengwa kwenye hilo bwawa alilolisema kwa ajili ya kurahisisha mawasiliano kati ya wananchi wa pande hizo mbili. (Makofi)