Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 182 2023-04-27

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa kivuko kipya ya Kigamboni utaanza baada ya kutengewa fedha mwaka 2022/2023?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GEDFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) katika mwaka wa fedha 2022/2023 umetenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa kivuko kipya katika Kituo cha Magogoni – Kigamboni.

Mheshimiwa Spika, uzoefu uliopatikana kwa kutumia vivuko vidogo (sea taxi) vilivyokodishwa toka Kampuni ya Azam Marine umeonesha kuwa vivuko hivyo vina ufanisi zaidi katika kutatua kero ya ucheleweshwaji wa abiria. Hivyo, Serikali imeamua

kununua vivuko vidogo viwili. Taratibu za manunuzi ya vivuko vidogo viwili kwa ajili ya abiria (Sea Taxi) ambavyo vitakuwa na uwezo wa kubeba abiria 250 kila kimoja zinaendelea, ahsante.