Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italifanya somo la kilimo kuwa la lazima kwenye Vyuo vya Ufundi?

Supplementary Question 1

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nitakuwa na swali moja la nyongeza. Kwa kuwa imethibitika pasipo shaka kwamba maendeleo sio miujiza. China wana Vyuo karibu 7,294 vya shule za ufundi. Je, sasa Serikali haioni umuhimu wa kuwa na Sera ya kuwa na vyuo kama ilivyokuwa kwenye Sera ya Afya kwamba kila Kata, sasa Sera hii iende kwenye kila jimbo na hasa majimbo ya vijijini ili tuwafundishe sasa watu wetu kulima katika maeneo madogo, tija kubwa pia ili waweze sasa kubadilisha udongo badala ya kuchoma majani wawe wanafukia? Ahsante sana.

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kiswaga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua sana umuhimu wa elimu ya mafunzo ya amali ambayo mara nyingi tunaita mafunzo ya ufundi stadi na ndio maana sasa hivi tume-register vyuo takribani 809, vya Serikali 77 na vingine vilivobaki ni vya watu binafsi na bado vile vile Serikali inaendelea na ujenzi wa Vyuo vya Ufundi stadi 65, kimoja cha Mkoa wa Songwe na Vingine 64 kwa ajili ya kila wilaya. Pamoja na hivyo kama ambavyo tutakuja kulieleza Bunge lako katika Semina ambayo tutakuja kukuomba, Mabadiliko ya Sera na Mitaala ambayo yanafanyika yataongeza ufundishaji wa elimu ya amali (ufundi stadi katika Shule za Serikali) ili kuhakikisha kwamba kweli tunaongeza ujuzi kwa wanafunzi wetu wanaohitimu, ahsante.