Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 181 2023-04-27

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali italifanya somo la kilimo kuwa la lazima kwenye Vyuo vya Ufundi?

Name

Prof. Adolf Faustine Mkenda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rombo

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Vyuo vya Ufundi Stadi kutoa mafunzo yanayozingatia shughuli za kiuchumi za maeneo husika na Taifa kwa ujumla ili kuwawezesha wananchi kutumia kikamilifu fursa na rasilimali zilizopo nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), imekuwa ikifanya upembuzi yakinifu kabla ya uanzishaji wa fani za ufundi ili kubaini mafunzo yanayofaa kutolewa katika vyuo hivyo kulingana na fursa na rasilimali zilizopo katika maeneo husika. Kozi ya kilimo ni miongoni mwa Kozi zinazotolewa katika Vyuo vya Ufundi Stadi vya Kihonda, Dakawa, Katavi, Arusha na Manyara. Aidha, katika Vyuo vipya 64 vya Wilaya vinavyojengwa, kutakuwa na karakana moja kwa kila

chuo kwa ajili ya kutoa mafunzo yatakayozingatia shughuli za kiuchumi katika eneo husika ikiwemo kilimo, nashukuru.