Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza, nina swali moja la nyongeza. Kwanza napenda niipongeze Serikali kwa majibu yake mazuri. Je, Waziri yuko tayari kwenda kukikagua Kituo hicho cha Polisi ambacho Waziri amesema kitamalizika Agosti, 2023?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, nimewahi kukitembelea kituo hiki na kuona kasi ya ujenzi unavyoendelea, inanitia moyo kwamba inaweza ikamalizika. Hata hivyo, kwa vile hakuna zida mbovu, niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge baada ya Bunge kukamilika ili kwenda kuangalia maendeleo ya ujenzi na kujiridhisha kwamba kitakamilika katika muda uliopangwa, nashukuru.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Maswa ni wilaya Kongwe katika Mkoa wa Simiyu, lakini haina Kituo cha Polisi kabisa. Ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Wilaya ya Maswa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, tunatambua uwepo wa baadhi ya wilaya kongwe kama ilivyo Maswa ambazo hazina Kituo cha Polisi. Mara kadhaa tumetoa ahadi hapa, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti zetu zinazofuata tutaangalia uwezekano wa kutenga fedha kwa ajili ya kuanza wa ujenzi wa Kituo cha Polisi ngazi ya wilaya katika Wilaya ya Maswa, nashukuru.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale pamoja na kwamba ni ya mwaka 1975 haijawahi kuwa na jengo la Kituo cha Polisi, lakini Serikali walituahidi kutujengea Vituo vya Polisi katika Kata za Kimambi, Lilombe na Kibutuka. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hii?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, tumewahi kueleza hapa na naomba nirudie kwamba katika wilaya zetu hasa kwenye kata, mpango wa Serikali ni ku- support pale ambapo juhudi zimeoneshwa na wananchi na halmashauri zao za ujenzi wa vituo hivyo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge akitusaidia kupitia Mfuko wa Jimbo, akaanzisha ujenzi, kwa vyovyote vile IGP kupitia fungu lake atatoa fedha za kusaidia kukamilisha vituo vyake. Kwa hiyo, nimtie moyo, hizi kata tatu ambazo zina changamoto za uhalifu, tuanze kwenye ngazi ya halmashauri na Mfuko wa Jimbo ili ngazi ya wizara kupitia Jeshi la Polisi liweze kusaidia kukamilisha, nashukuru.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 4

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushuru. Wananchi wa Kata ya Mazinde kwa kushirikiana nami Mbunge wao tumeshirikiana kujenga Kituo cha Polisi mpaka boma limekamilika. Je, ni lini Serikali itatusaidia kumaliza Kituo hicho cha Polisi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, kupitia bajeti ya mwaka 2023/2024, tutaona uwezekano wa kupata fedha kutoka Mfuko wa Tuzo na Tozo kukamilisha Kituo cha Mazinde ambacho Mheshimiwa Mbunge amekizungumzia.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 5

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante. Polisi wote nchini wanapitia Shule ya Polisi Moshi inayojulikana kama CCP, shule hiyo ni chakavu, mbovu, barabara hazipitiki na wakija wageni wanapitishwa kwenye geti kubwa na sio hili la Moshi Sekondari. Je, ni lini sasa Serikali itakarabati chuo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, nimekitembelea Chuo cha Polisi Moshi na kubaini uchakavu anaousema na kupitia ziara yangu tulikubaliana na uongozi wa Manispaa ya Moshi kupitia Mamlaka ya Barabara za Mjini na Vijijini (TARURA) kwa sababu chuo hiki kipo kwenye himaya yake waanze kutenga fedha. Nimtie moyo Mheshimiwa Mbunge kwamba, barabara kuu inayoingia tayari ukarabati umefanyika na tutaendelea kufanya ukarabati huo kwenye barabara zote nyingine zilizopo kwenye chuo hicho, nashukuru.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 6

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kituo cha Polisi Kwamtoro ni kituo cha majengo ya mkoloni, kimechakaa, hakitamaniki, hakithaminiki. Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, kulingana na upatikanaji wa bajeti tunaendelea kuvikarabati Vituo vyote vya Polisi vilivyochakaa. Hiki cha Kwamtoro pia tutakiingiza kwenye mpango wa matengenezo kadri tutakavyopata fedha kutoka Serikalini, nashukuru.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 7

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa. Kutoka Makambako mpaka unaingia Mafinga hali ya usalama sio nzuri kwa sababu hakuna Kituo cha Polisi na tayari jitihada zimekwishaanza kufanywa na wananchi kwa kutenga eneo na hata mimi mwenyewe Mbunge kupeleka cement. Je, Wizara iko tayari kupeleka fedha kuhakikisha kwamba Kituo cha Polisi cha Nyololo kinakamilika?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, kwa jitihada ambazo zimekwishafanywa na Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wake wizara itamuunga mkono kukamilisha kituo hicho, nashukuru.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 8

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, ahsante. Gari lililopo katika Kituo cha Polisi Magugu ni chakavu. Je, ni lini Serikali itawapatia kituo hicho gari ili kurahisisha utendaji kazi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, tunao mpango katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Jeshi la Polisi kununua magari na kuzipatia Wilaya zote za Kipolisi nchini Tanzania. Naamini gari hiyo itakapopatikana, basi magari yaliyopo kwenye ngazi ya wilaya yanaweza kupelekwa kwenye kituo hicho kama kutaonekana kuna uhitaji mkubwa wa gari, nashukuru.

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Supplementary Question 9

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mtwara Mjini ndio kwenye Kituo Kikuu cha Polisi. Kituo hicho kilijengwa toka mwaka 1962, kwa sasa kituo hicho ni chakavu mno na inapelekea Askari kufanyia kazi kwenye mwembe. Je, ni lini Serikali itakwenda kufanya ukarabati kwenye kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, tunatambua hali ya uchakavu wa Kituo cha Polisi ngazi ya Wilaya Mtwara. Hata hivyo, katika bajeti yetu ya mwaka 2023/2024, fedha zimetengwa za kuanza kufanya ukarabati kwenye kituo hicho. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge awe na matumaini kwamba mwaka 2023/2024 kituo hicho kitakarabatiwa, nashukuru.