Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 14 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 179 2023-04-27

Name

Maryam Azan Mwinyi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI: aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakarabati upya Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Mkoani Pemba pamoja na nyumba za kuishi askari wa kituo hicho?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Azan Mwinyi Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Jengo la kituo cha Polisi cha wilaya ya Mkoani, mkoa wa kusini Pemba ni chakavu na halifai kwa matumizi ya kutoa huduma za Polisi. Mwezi Disemba 2022 Serikali imetoa kiasi cha fedha shilingi milioni 700 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi kipya cha Daraja B eneo hilo. Taratibu za ujenzi zimeshaanza na ujenzi unatarajia kukamilika mwezi Agosti, 2023.

Mheshimiwa Spika, tathimini ya uchakavu kwa ajili ya kufanya ukarabati wa nyumba ya makazi ya askari ya kuishi familia nne ambayo iko eneo la kituo imeshafanyika na kubaini kwamba shilingi milioni 46.27 kinahitajika kwa ajili ya kubadilisha paa, dari, miundombinu ya maji safi, maji taka na umeme, kuziba nyufa na kupaka rangi. Fedha hizo zitaombwa kutoka kwenye mfuko wa tuzo na tozo katika mwaka wa fedha 2023/2024.