Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tamima Haji Abass

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TAMIMA HAJI ABASS aliuliza: - Je, kuna utafiti uliofanywa na Serikali kujua sababu za uwepo wa Watoto wa mitaani?

Supplementary Question 1

MHE. TAMIMA HAJI ABASS: Mheshimiwa Spika, ahsante sana pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; baada ya kutambua sababu za uwepo wa watoto hao, Je, Serikali ina mpango gani? Swali la pili kwa kuwa mikoa iliyofanyiwa utafiti huo ni michache; Je, Serikali ina mpango wa kuendelea na utafiti kama huo? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika,napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tamima kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea na mikakati endelevu kutoa malezi bora kwa wazazi na mafunzo ili kuwatunza watoto katika ngazio ya familia lakini itafanya iwakutanishe watoto hao na wazazi wao. Watoto wasio na wazazi watapata huduma na haki zote stahiki katika vituo vyetu vya watoto tunavyolelea watoto yaani, Kikombo – Dodoma na Kurasini – Dar es Salaam lakini pia tutaimarisha ulinzi na usalama kwa watoto hao.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, Serikali itaendelea kufanya tafiti mbalimbali katika mikoa ambayo inachangamoto za mitaani ili kuhakikisha usalama wao. Lakini pia nitoe rai kwa wazazi na walezi kuhakikisha wanakaa na familia yao familia za watoto wao ili kuhakikisha wanapata malezi bora. Pia mtoto wa mwenzio ni wako, na watoto wote wanastahili kupewa haki muhimu kwa vile mtoto wa leo ni Taifa la kesho, ahsante. (Makofi)