Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: - Je, Serikali kwa kushirikiana na Wahisani ina mpango gani mahsusi wa kutoa Bima za Afya bure kwa watu wenye Ulemavu wa kudumu?

Supplementary Question 1

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana Serikali kwa majibu mazuri na mipango mizuri na mikakati mizuri kwa ajili ya Bima ya Afya kwa watu wote. Naomba niulize swali langu la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunafahamu kwamba watu wenye ulemavu ni watu ambao hawajiwezi wengine. Je, Serikali haioni haja sasa ya kuweka dirisha maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu kama vile kwa Wazee?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Kwa kuwa Bima ya Afya mara nyingine vipimo vingine havifanyiki. Je, Serikali haioni haja sasa kwamba vipimo vya Kansa ya Saratani ya Ngozi viweze kufanyika bure katika hizo Bima ambazo mnaziandaa kuja? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Spika, moja amesema kuwa na dirisha maalum kwa ajili ya watu wenye Ulemavu. Hili ni wazo zuri sana tunalichukua, vilevile pamoja na kuwa na dirisha lakini ni katika kila infrastructure ya hospitali kwenye wodi na kila mahali kuwepo na sehemu ambazo ni maalum zinazowezesha watu wenye ulemavu kuweza kupata huduma kirahisi kama wanavyopata watu wengine.

Meshimiwa Spika, nimeona vilevile amezungumzia na watu wenye ulemavu wa ngozi. Sasa hivi kwa mfano kwenye Hospitali ya Kanda ya KCMC wamepelekwa watu kutoka Hospitali mbalimbali za Mikoa. Moja kujifunza kwa ajili ya kuzalisha dawa maalum kwa ajili ya wale watu wenye ulemavu wa ngozi hasa ile screening ile ya kujipaka kwa ajili ya kuzia miale ya jua. Kwa hiyo, hayo yanaboreshwa na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni suala la kwamba kuna baadhi ya mahitaji ambayo ya kitiba ambayo wanahitaji baadhi ya Walemavu ambayo hayapo kwenye Mfuko wa Bima ya Afya. Mheshimiwa Mbunge kwa sababu tunaenda kuboresha kuja na Muswada wa Bima ya Afya kwa watu wote, ni wakati wa muafaka wa sisi kuhakikisha kwamba vitu vyote hivyo vimeingia kwenye utaratibu. Lakini wakati kabla hatujafikia hilo la Sheria ya Mfuko wa Bima ya Afya, naomba mimi na wewe tukae unianishie hayo mambo maalum ili Mheshimiwa Waziri wa Afya aweze kuyafanyia kazi mapema, ahsante. (Makofi)

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: - Je, Serikali kwa kushirikiana na Wahisani ina mpango gani mahsusi wa kutoa Bima za Afya bure kwa watu wenye Ulemavu wa kudumu?

Supplementary Question 2

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, ahsante, nakushukuru kwa kuniona. Kwa kuwa Serikali ilikuwa na mpango wa Bima za Afya kwa wote, je, ni hatua ipi imefikiwa ili kupata Bima hizo? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, hatua zilizofikiwa. Kwanza zimefikiwa hatua zote za kitaalam, tuko kwenye hatua ambayo nafikiri uliona Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Waziri wa Afya alileta ushauri wake na akawaleza Wabunge hatua tuliyofikia ambavyo Wabunge mmetoa input muhimu na mmeturuhusu tuendelee na mchakato.

Kwa hiyo, hatua ambayo tunaendelea sasa ni zile hatua ambazo kwa kweli inatakiwa maoni yenu Wabunge nasi pamoja Serikali na Wabunge tuweze kulisukuma na Muswada huo uje mapema Bungeni. Kikubwa tunategemea mchango wenu mzuri ili mwisho wa siku tukishapitisha basi pasiwepo na kasoro ambazo tutaziona baadae.(Makofi)

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: - Je, Serikali kwa kushirikiana na Wahisani ina mpango gani mahsusi wa kutoa Bima za Afya bure kwa watu wenye Ulemavu wa kudumu?

Supplementary Question 3

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Sambamba na Bima kwa Walemavu umezuka ugonjwa kwa wanawake wanaojifungua watoto ambao wana mgongo wazi, hasa kule Mkoa wa Mbeya kwenye Hospitali ya Rufaa pale wanachaji fedha kuanzia 500,000 mpaka 1,000,000. Je, Serikali ina mpango gani kuwasaidia kuwapunguzia mzigo wa kulipa gharama hizo wanawake wanaojifungua watoto wa mgongo wazi? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza Mheshimiwa wa Waziri wa Afya alishaelekeza na ameshasema mara nyingi kwamba akina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano wanatakiwa wapate huduma bure, hilo ni la kwanza. Lakini ninyi ni mashahidi Waheshimiwa Wabunge jinsi ambavyo Serikali imeendelea kuboresha infrastructure kwa miaka sasa mingi sasa hivi tunaenda ndani ya miezi miwili hakutakuwepo na hospitali ya Mkoa haina na CT scan na vile vifaa ambavyo vitatusaidia kufanya operation zile ambazo zinahitaji utaalam wa juu kama hizo. Kwa hiyo kikubwa ni kwamba tutaboresha hiyo, ili iwe inaenda sambamba na suala la watoto njiti. Kwa hiyo watoto njiti na hao wanaozaliwa na malformation mbalimbali imewekwa utaratibu na ma-specialist wanapelekwa kwenye maeneo kwa ajili ya kuhakikisha hilo.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge mkikutana na matatizo specific kwa sababu binaadam ndiyo wale wale mnatuambia mimi na Waziri na hata information kutoka popote zinafanyiwa kazi kwa wakati wake. Ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: - Je, Serikali kwa kushirikiana na Wahisani ina mpango gani mahsusi wa kutoa Bima za Afya bure kwa watu wenye Ulemavu wa kudumu?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushuru. Kuna utafiti ulifanywa na Jumuiya ya Viongozi wa Dini kuhusiana na mambo ya Bima ambao unaonyesha takribani Watanzania milioni 15 hawana uwezo wa kabisa wa kujikatia hii Bima ya Afya.

Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuweza kuwakatia hawa Watanzania Milioni 15 waweze kupata matibabu wakati huo wakisubiria Bima ya Afya? (Makofi)

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali zuri la Mbunge. Kwanza, moja kupanga ni kuchagua na tunaopitisha bajeti ni sisi, kwa hiyo kikubwa tayari Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu imejulikana kweli kwamba kuna asilimia 28 ya watu ambao hawawezi kujilipia, Rais wetu ameshakubali itengwe kila mwaka bilioni 149.77 kwa ajili ya kuwahudumia watu hao ambao unasema.

Mheshimiwa Spika, wakati tunapanga nikuambie tu ni rahisi sana kungojea wewe LUKU iingie kwenye nyumba ukaacha kuwa na giza lakini ukiugua haisubiri. Kikubwa tunachowaambia wakati wa kupanga na kuamua vipaumbele tukate kodi wapi hasa kwenye Bima ni wakati wa sisi Wabunge kuchagua tunaelekea upande gani.

Mheshimiwa Spika, ahsanteni sana. (Makofi)