Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 23 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 203 2022-05-16

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA S. TAYA aliuliza: -

Je, Serikali kwa kushirikiana na Wahisani ina mpango gani mahsusi wa kutoa Bima za Afya bure kwa watu wenye Ulemavu wa kudumu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya naomba kujibu swali la Mheshimiwa Khadija Shaaban Taya Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sera ya Afya imetoa utaratibu wa kusaidia watu wenye mahitaji maalum wasio na uwezo. Hata hivyo Serikali inakamilisha Muswada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote ambapo utawezesha watu wote wakiwemo watu wenye ulemavu kupata huduma katika vituo mbalimbali vinavyotoa huduma za afya, ahsante.